METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, December 19, 2019

WADAU WA MAENDELEO WAPONGEZWA KUFANIKISHA MPANGO WA KILIMO WA KUHIMILI MABADILIKO YA TABIA NCHI (ACRP)


Mkurugenzi wa Mafunzo na Utafiti Wizara ya Kilimo Dkt.Wilhelm Mafuru akitoa hotuba ya ufunguzi kwa niaba ya Katibu Mkuu
Wajumbe wa kikao cha Kutathmnini Mpango wa Kilimo wa Kuhimili Mabadiliko ya tabia nchi mara baada ya ufunguzi Jijini Dar es Salaam 
Wajumbe wa kikao cha Kutathmnini Mpango wa Kilimo wa Kuhimili Mabadiliko ya tabia nchi mara baada ya ufunguzi Jijini Dar es Salaam 

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe amewapongeza wadau wa maendeleo wa ndani na nje kwa kufanikisha Mpango wa  Kilimo wa Kuhimili Mabadiliko ya tabia nchi (ACRP)

Pongezi hizo zimetolewa leo jijini Dar es Salaam na Dkt.Wilhelm Mafuru Mkurugenzi wa Mafunzo na Utafiti Wizara ya Kilimo alipofungua kikao cha tathmni ya Mpango kwa niaba ya Katibu Mkuu

"Wizara ya Kilimo imefanikisha Mpango huu wa Kuhimili mabadiliko ya tabia nchi kwa kuhamasisha Kilimo kinachojali na kulinda mazingira kwa ushirikiano na wadau" alisema Dkt Mafuru

Aliongeza kusema Mpango huo ulianza kutekelezwa na Wizara mwaka 2014 na unafikia mwisho mwaka huu 2019 ambapo lengo kuu la Mpango lilikuwa kuhakikisha nchi inaongeza uzalishaji wa mazao na usalama wa chakula.

Mpango huu unahamasisha wakulima kutumia eneo dogo kuzalisha mazao mengi kwa tija wakizingatia matumizi sahihi ya teknolojia na hifadhi ya mazingira .

Dkt.Mafuru ametaja maeneo ya kipaumbele yaliyotekelezwa kwenye Mpango wa kilimo cha Kuhimili mabadiliko ya tabia nchi (ACRP) kuwa ni kuboresha matumizi ya ardhi na maji,kuchochea matumizi ya Kilimo kinachokabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na tatu kupunguza madhara ya athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Utekelezaji huu wa Mpango umezingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo (2025),Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ( 2020) na Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II).

Naye Mshauri wa Mazingira na Uhifadhi wa Mali asili toka Ubalozi wa Norway nchini Ingvild Langhus amesema Kilimo kinachohilimi mabadiliko ya tabia nchi kinasaidia kuondoa uchafuzi wa hali ya hewa na mazingira.

Amesema Norway kwa zaidi ya miaka Arobaini imekuwa ikishirikiana na serikali ya Tanzania katika kuinua sekta ya Kilimo hususan utafiti.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa kitengo cha Mazingira Wizara ya Kilimo Prosper Makundi amesema Mpango huu kutokana na mafanikio yaliyofikiwa nchini ni budi wadau na wahisani wakaona namna ya kuongeza ufadhili ili awamu ya pili ya ACRP ianze.

"Baada ya kikao hiki ni mategemeo ya wizara kuona wadau wetu wanaongeza ufadhili ili kazi ya kusimamia na kuelimisha wakulima kilimo kinachohilimi mazingira iendelee awamu ya pili" alisema Makundi.

Kikao kimeandaliwa na.Wizara ya Kilimo na kushirikisha na wadau toka Ofisi ya Makamu wa Rais ,Mazingira.Wizara ya Ardhi.SUA,FAO,WB,Care International, FORUMCC,IITA na ANSAF

Mwisho.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com