Monday, April 1, 2024
Wednesday, March 6, 2024
KADA WA CCM NEEMA MGHEN ACHANGIA MIFUKO 50 UJENZI WODI YA WAZAZI USHETU
Wednesday, February 21, 2024
UTEKELEZAJI MRADI WA TANZANIA YA KIDIJITALI WAFIKIA 70%-KATIBU MKUU WHMTH, MOHAMMED KHAMIS ABDULLA
Monday, February 19, 2024
TUNATEGEMEA MAFANIKIO MAKUBWA REA – BODI MPYA
Na Veronica Simba – REA
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) inayosimamia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imesema inategemea mafanikio makubwa katika kuiwezesha Wakala hiyo kutimiza azma yake ya kuwafikishia wananchi walioko vijijini nishati bora za umeme, mafuta na gesi.
Hayo yamebainishwa mwishoni mwa wiki na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Balozi, Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu baada ya kikao cha kwanza cha Bodi hiyo mpya kilicholenga kutambuana na kupanga majukumu.
“Kikao chetu kimeenda vizuri, tumechagua Kamati na kupangiana majukumu. Tunaamini na tunaahidi kuwa tutatekeleza majukumu yetu sawasawa na Sheria iliyoanzisha Wakala wa Nishati Vijijini inavyoelekeza,” amesema.
Aidha, Balozi Kingu amemshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumteua kuwa Mwenyekiti wa Bodi na amemshukuru Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ndiye Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko kwa kukamilisha mchakato wa uteuzi wa Wajumbe wa Bodi, jambo ambalo limeiwezesha kuwa Bodi kamili.
Akieleza zaidi kuhusu majukumu waliyojipangia, Balozi Kingu amesema mapema Mwezi Machi, Bodi itakutana katika kikao cha dharura kupitia na kujadili masuala mbalimbali ya Wakala ambayo yalikuwa yakisuburi baraka za Bodi ili kuyatolea maamuzi yatakayowezesha utekelezaji wake kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla.
Kwa upande wake, Katibu wa Bodi hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa REA, Mhandisi Hassan Saidy amepongeza Mamlaka za Uteuzi, kuteua watu makini, hodari na wachapakazi ambao amesema ni muhimu kuwa nao katika kuisimamia Wakala hiyo yenye majukumu makubwa yanayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja.
“REA ina jukumu kubwa ambalo linagusa maisha ya watu lakini pia linahusisha kiasi kikubwa sana cha fedha za Serikali. Kwahiyo, kuwa na Bodi nzuri iliyosheheni watu makini, kwetu sisi ni jambo la faraja,” amefafanua.
Mkurugenzi Mkuu, kwa niaba ya Menejimenti na Wafanyakazi wote wa REA, ametoa ahadi ya ushirikiano kwa Bodi hiyo mpya ili kuhakikisha malengo ya Serikali kupitia majukumu yaliyokasimiwa kwa Wakala yanatekelezwa.
“Tunatamani kuona Watanzania wenzetu wanaoishi vijijini wanapata nishati bora kama ilivyo kwa wenzao wanaoishi mjini,” amesisitiza.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Wajumbe wa Bodi wamezishukuru Mamlaka za Uteuzi kwa kuwaamini na kuwapa jukumu hilo kubwa la kuisimamia REA ili kuendelea kuleta matokeo chanya.
Aidha, wamepongeza Bodi zilizotangulia kabla yao, Menejementi pamoja na Wafanyakazi wote kwa kazi nzuri waliyofanya tangu kuanzishwa kwa Wakala na kuahidi kuendeleza yote mazuri yaliyofanyika ili kuongeza tija.
Kikao hicho pia kilishirikisha Menejimenti ya Wakala ambapo Wakuu wa Idara na Vitengo waliwasilisha kwa Bodi taarifa za utekelezaji wa majukumu katika maeneo wanayosimamia kwa lengo la kuijengea Bodi uelewa na ufahamu kuhusu Taasisi hiyo waliyopewa jukumu la kuisimamia.
Januari 26 mwaka huu, Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko aliwateua Florian Otman Haule, Lucas Charles Malunde, Mwantum Issa Sultan, Stephen Menard Mwakifamba, James Issack Mabula, Ahmed Martin Chinemba, Sophia Shaban Mgonja na Balozi Radhiya Naima Msuya kuwa Wajumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini, wakiungana na Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Gideon Kingu aliyeteuliwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, Septemba 2023 kuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo.
Serikali, Benki ya Dunia wakutana kujadili mradi wa Tanzania ya Kidijitali
Friday, February 16, 2024
MBUNGE OLE LEKAITA AKABIDHI MAGARI MAWILI YA WAGONJWA KITUO CHA AFYA SUNYA-KITETO
MBUNGE NYONGO AIGEIKUIA SERIKALI KUNUNUA PAMBA SOKO LINAPOPOROMOKA
Thursday, February 15, 2024
JE, SERIKALI INAMKAKATI GANI WA HARAKA KUHAKIKISHA MIUNDOMBINU YA TAZARA INAKUWA KIWANGO CHA SGR?"MBUNGE NJEZA"
Na Saida Issa, Dodoma
SERIKALI INAENDELEA NA UPEMBUZI YAKINIFU NA USANIFU BONDE LA BUYUNGU.
Na Saida Issa, Dodoma
Wednesday, February 14, 2024
TANZANIA KUWA NCHI YA 22 AFRIKA KUFANYA UTAFITI WA GHARAMA ZA UTAPIAMLO NCHINI-MHE UMMY NDERIANANGA
Thursday, February 8, 2024
SERIKALI KUENDELEA KUWAINUA KIUCHUMI VIJANA WENYE ULEMAVU
SERIKALI YAOMBWA KUAJIRI WALIMU ILI KUENDANA NA IDADI KUBWA YA WANAFUNZI- MBUNGE KAKONKO KAMAMBA.
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
📌 Asema Rais, Dkt. Samia anafanya kazi kubwa ya kuwaunganisha Watanzaia 📌 Atak...
-
Timu inayoundwa na Wana-Diaspora wa Kitanzania waishio Sweden, Kilimanjaro FC, hivi karibuni imefanikiwa kupanda daraja kutoka Daraja ...
-
Leo Septemba 29, 2017 Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo John L.Kayombo amemkabidhi mkandarasi kazi ya kujenga daraja litakalounganisha maen...
-
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Ofisa Ushirika wa Manispaa ya Musoma Bibi Yunia Wiga kufuatilia up...
-
Mbunge wa Ushetu Mhe. Emanuel Cherehani akizungumza na wadau na wa chama katika Mkutano Mkuu wa nne wa Chama Kikuu cha Ushirika Milambo k...