
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akiwa kwenye picha ya pamoja na wananchi wa Kijiji cha Nkui, sawia na baadhi ya wajumbe wa kamati ya siasa ya Wilaya ya ikungi mara baada ya kumalizika kwa mgogoro
Dc Mtaturu akisisitiza jambo wakati wa kikao cha maridhiano
Dc Mtaturu akielezea faida ya mradi wa
umeme wa Kilovolti 400 njia ya Iringa- Shinyanga
Dc Mtaturu akizungumza na wananchi waliofika kumlaki baada ya kusikia amezuru kijijini hapo
Umakini unahitajika kutekeleza dhana ya Hapa Kazi Tu
Na Mathias Canal, Singida
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu amemaliza mgogoro baina ya serikali ya
kijiji cha Nkui kilichopo Kata ya Issuna pamoja na mwananchi Jonas Martin Bahali uliodumu kwa zaidi
ya mwaka mmoja sasa dhidi ya Tanesco katika mradi wao wa umeme wa Kilovolti 400
njia ya Iringa- Shinyanga.
Kikao hicho cha pamoja kwa ajili ya maridhiano kimeimarisha uelewano kati ya
kijiji na mwananchi huyo ambaye kwa kiasi kikubwa hakupatiwa elimu nzuri juu ya
umuhimu wa mradi huo kwa Wilaya ya Ikungi, Mkoa,Taifa na kwa mwananchi mmoja
mmoja kuelekea Tanzania ya viwanda kwani ndio umeme wenye uwezo mkubwa kuhimili
viwanda vikubwa nchini.