METDO Tanzania

METDO Tanzania
Showing posts with label Siasa. Show all posts
Showing posts with label Siasa. Show all posts

Tuesday, November 6, 2018

Saturday, August 20, 2016

JK AONGOZA MAZISHI YA MWANAMUZIKI SHAKILA SAID

wa
Rais Mstaafu awamu ya nne,Dkt Jakaya Kikwete akiweka saini kitabu cha maombolezo cha Bi Shakila Said ,huko nyumbani kwake Mbagala Charambe,jijini Dar,wa pili kushoto akishuhudia ni Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh.Nape Nnauye.

Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akiweka saini kitabu cha maombolezo cha Bi Shakila Mbagala Charambe,jijini Dar,kushoto ni  Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh.Nape Nnauye.
 
Mke wa Rais Mstaafu awamu ya nne,Mama Salma Kikwete akiweka saini kitabu cha maombolezo cha Bi Shakila Said ,huko nyumbani kwake Mbagala Charambe,jijini Dar.

CHANZO :MICHUZI BLOG
Share:

Watumishi hewa Wameongezeka na Kufikia 16,127

TAARIFA rasmi ya mwisho ya utekelezaji wa kuwaondoa watumishi hewa serikalini na taasisi zake zote, itawasilishwa kwa Rais John Magufuli Ijumaa wiki ijayo na kwamba hadi sasa wameshabainika watumishi hewa 16,127 na wameondolewa kwenye mfumo wa utumishi.

Aidha, mbali ya serikali kuokoa Sh bilioni 16.15 kwa mwezi huu wa Agosti baada ya watumishi hewa hao kuondolewa kwenye mfumo wa utumishi, ambao kama wasingeondolewa fedha hizo zilikuwa ziwalipe mshahara, posho na malipo mengine, waajiri 145 hawajawasilisha taarifa kuhusu uhakiki wao.
Share:

Friday, August 19, 2016

Sababu za Kutumbuliwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Hizi Hapa

Daudi Felix Ntibenda jana asubuhi alikuwa na majukumu ya kufungua mikutano miwili na kufanya shughuli nyingine kwa nafasi yake ya mkuu wa Mkoa wa Arusha, lakini hakuweza kuyatimiza kikamilifu majukumu hayo kwa kuwa Rais John Magufuli alikuwa na mawazo tofauti na mipango yake.

Ingawa haikufahamika sababu ya kuondolewa kwake, huenda mvutano baina yake na Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa ukawa umechangia.
Share:

Thursday, August 18, 2016

DC MTATURU AMALIZA MGOGORO ULIOCHELEWESHA MRADI WA UMEME WA KILOVOLTI 400

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akiwa kwenye picha ya pamoja na wananchi wa Kijiji cha Nkui, sawia na baadhi ya wajumbe wa kamati ya siasa ya Wilaya ya ikungi mara baada ya kumalizika kwa mgogoro
 Dc Mtaturu akisisitiza jambo wakati wa kikao cha maridhiano
 Dc Mtaturu akielezea faida ya mradi wa umeme wa Kilovolti 400 njia ya Iringa- Shinyanga
 Dc Mtaturu  akizungumza na wananchi waliofika kumlaki baada ya kusikia amezuru kijijini hapo
Umakini unahitajika kutekeleza dhana ya Hapa Kazi Tu

Na Mathias Canal, Singida

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu amemaliza mgogoro baina ya serikali ya kijiji cha Nkui kilichopo Kata ya Issuna pamoja na mwananchi Jonas Martin Bahali uliodumu kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa dhidi ya Tanesco katika mradi wao wa umeme wa Kilovolti 400 njia ya Iringa- Shinyanga.

Kikao hicho cha pamoja kwa ajili ya maridhiano kimeimarisha uelewano kati ya kijiji na mwananchi huyo ambaye kwa kiasi kikubwa hakupatiwa elimu nzuri juu ya umuhimu wa mradi huo kwa Wilaya ya Ikungi, Mkoa,Taifa na kwa mwananchi mmoja mmoja kuelekea Tanzania ya viwanda kwani ndio umeme wenye uwezo mkubwa kuhimili viwanda vikubwa nchini.
Share:

Tundu Lissu Atumia Dakika 120 Kupangua hoja Mahakamani


Tundu Lissu, ambaye ni wakili wa Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya jana alitumia muda wa saa mbili kupangua maombi ya wananchi wanne wanaopinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu yaliyompa ushindi mteja wake. 
Kesi hiyo imeanza kusikilizwa tena baada ya Mahakama ya Rufaa kufuta uamuzi wa Mahakama Kuu uliotupilia mbali hoja za kupinga matokeo hayo, ambazo ziliwasilishwa na wafuasi wanne wa aliyekuwa mgombea wa jimbo hilo, Steven Wasira (CCM). 
Jaji Mohamed Gwae wa Mahakama Kuu, alitupilia mbali kesi hiyo baada ya kukubali pingamizi la Lissu kuwa wafuasi hao hawakuwa na haki ya kisheria kufungua kesi hiyo. 
Share:

Tuesday, August 16, 2016

Chama cha Wakulima (AFP) chalaani maandamano ya UKUTA

index

Na Maelezo-Zanzibar

Chama cha Wakulima (AFP) kimelaani vikali dhidi ya hujuma zilizoandaliwa kufaywa na Umoja wa Wananchi UKAWA ifikapo tarehe 1mwezi ujao.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mwenyekiti wa Chama hicho Said Soud Said katika Ukumbi wa Sanaa uliopo Rahaleo Zanzibar amesema hujma hizo zilizoandaliwa na UKAWA za kufanya maandamano makubwa ya kupinga Serikali iliopo madarakani zilizopangwa nchi nzima zina lengo la kuvuruga amani nchini.
Share:
Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com