METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, October 6, 2019

DKT TULIA ATUNUKIWA UANACHAMA WA SHIRIKA LA MSALABA MWEKUNDU





Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson ametunukiwa Uanachama wa maisha na Shirika la Msalaba Mwekundu nchini (Tanzania Red Cross).

Dkt Tulia ametunukiwa uanachama huo leo tarehe 6 Octoba 2019 katika Mkutano wa Taifa wa Shirika hilo uliofanyika Jijini Dodoma baada ya kukubali kuwa Balozi.

Dkt. Tulia amesema “Niwashukuru kwa ombi hili zito mlilonipa na nilipokee kwa unyenyekevu kabisa kwa kusema kwamba nimekubali kuwa balozi wa kudumu na nitafanya kazi hiyo kwa uaminifu kabisa”

“Niwatakie kila la kheri Viongozi wote na Wanachama wa Red Cross, Wakati sisi tunakua ilikuwa tukiliona gari la Red cross tulikuwa tunakimbia mbio kwa sababu ilikuwa inaonekana kana kwamba ni wanyonya damu, lakini mambo haya yameisha kwenye jamii kwasababu ya kazi kubwa na nzuri mnayoifanya kwa jamii ikiwemo kutoa elimu na watu wamefahamu kwamba nyie sio wanyonya damu bali ni watoa huduma za kibinadamu” Alisema Dkt. Tulia

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com