METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, September 23, 2017

JAFO APONGEZA USHIRIKIANO WA WADAU KATIKA KULETA MAENDELEO NCHINI

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akizungumza katika uzinduzi wa mpango mkakati wa Tanzania Evaluation Association
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akizindua mpango mkakati wa Tanzania Evaluation Association
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akizindua mpango mkakati wa Tanzania Evaluation Association

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tamisemi Mhe. Selemani Jafo amepongeza wadau mbalimbali nchini kwa kuendelea kushirikiana na serikali katika kuleta maendeleo ya Taifa.

Jafo aliyasema hayo alipokuwa akizindua Mpango mkakati asasi ya watathimini nchini uitwao Tanzania Evaluation Association (TanEA) uliofanyika Julius Nyerere Conference Centre jiji Dar es salaam.

Taasisi hiyo imefanikiwa kuzindua mpango mkakati huo wa miaka mitano kuanzia 2017 - 2021 ambao unalenga kufanya tathmini ya mipango mbalimbali ya maendeleo nchini ili kuweza kutoa mwanga kwa maeneo yaliyo fanyika vizuri na maeneo ambayo hayakupata mafanikio yaliyo kusudiwa ili kuiwezesha Tanzania kutimiza dhamira ya kufikia nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025 kupitia uchumi wa viwanda.

Akizungumza katika uzinduzi huo Jafo amezitaka taasisi mbalimbali hapa chini pamoja na taasisi za kimataifa kuendelea kushirikiana na serikali katika kuleta maendeleo hapa nchini.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com