METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, December 8, 2016

JAPAN WAWADAI ARDHI MAREKANI

AMINI NYAUNGO

Marekani moja ya nchi yenye ujanja sana haswa katika swala zima la kijeshi wanambinu nyingi sana haswa inapotokea vita , Japan pia miongoni mwa nchi zilizo vizuri swala zima la kijeshi,  Marekani walichokifanya kuomba hifadhi ya ardhi kwa ajiri ya watu wake wakijeshi kufanya mazoezi.

Miaka mingi sasa imepita tangu Marekani iombe kipande cha ardhi kwa ajiri ya wanajeshi na sasa miaka 20 imepita tangu wachukue, Japan sasa wanataka ardhi yao, Marekani inataraji kurejesha kipande cha ardhi cha Okinawa kwa Japan kinachosemekana kuchukuliwa na nchi hiyo miaka ishirini iliyopita.5846bcef12a3c-1

Eneo hilo limekua likitumika na jeshi la polisi la Marekani kwa mazoezi mbalimbali ya kijeshi na baada ya eneo hilo kurudishwa kwa wenye nalo wanajeshi wote watatakiwa kurudi Marekani. Wananchi wa eneo hilo wamekua wakilalamika juu ya uhamiaji wa jeshi la Marekani katika eneo hilo kwa muda mrefu sana hivyo kuwazuia wakazi hao kufanya kazi za kimaendeleo  kuongeza kipato chao.

Kutokana na masharti yaliyowekwa na Marekani,Japan inatakiwa ijenge sehemu kubwa ya kutua helikopta za kimarekani chini ya utawala wa Wamarekani wenyewe. Sharti hilo limepingwa na wengi kupelekea kusababisha kusitishwa kwa shughuli hiyo hadi pale polisi walipoingilia kati na kupambana na maandamano hayo.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com