Na Hamis Hussein -
Singida
Serikali
imetoa shilling bilioni 5.9 kwaajili ya kuendeleza ujenzi wa majengo mapya ya hospitali ya rufaa ya mkoa wa Singida ambayo itarahisisha huduma
mbalimbali afya ikiwemo upasuaji , tiba
za kibingwa na kupunguza gharama za
matibabu kwa wananchi kufuata huduma hizo
hospitali zingine za mbali kama
Benjamini Dodoma , au muhimbili.
Waziri
wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dr Doroth Gwajima ametembelea
kukagua ujenzi huo akiwa kwenye
ziara ya
kikazi
na kuridhishwa ujenzi huyo baada
ya
kuona umefikia
asilimia 70
ikiwa ni
awamu ya kwanza ya fedha zilizotengwa .
DR.
Gwajima alisema kukamilika kwa hospitali hiyo kutasaidia kuruhusu wodi za hospitali ya rufaa ambayo
majengo yake yameshachakaa kuhamishiwa
kwenye majengo mapya ambayo yanajengwa eneo la mandewa pamoja na
kurahisisha huduma za afya kwa jamii.
“Kutoka singida
nimekuja ziara fupi kuangalia maendeleo ya ujenzi wa hospitali mpya . iliyopo sasahivi
ile hospitali iliyopo katikati ya mji imebanwa majengo yake yamepitwa na wakati
, umefika wakati wa kuongeza kasi ili huduma za rufaa zihamie hospitali
mpya ya mandewa ambayo ni ya kisasa. Serikali
haiko nyuma imeshatenga na kuleta shilingi bilioni 5.9 . Jengo lote linavyooneka
hapa ni kubwa kuna sehemu ya upasuaji , maabara na wodi
mbalimbali . hii itaruhusu wodi za kule zilizobanana kuhamia huku na majengo ya hospitali ile yatumike na
halmashauri na hospitali hii itakapo
kamilika itatoa nafuu kwa hospitali ya Benjamini mkapa pamoja na gharama za
kwenda kutibiwa mbali ”.
amesema Dr. Doroth Gwajima.
Wakati
akikagua ujenzi wa majengo mapya ya hospitali Waziri Doroth Gwajima ametoa
maagizo kwa viongozi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa singida pamoja na
watendaji wengine kutoka serikalini kuundwa kwa kamati mbalimbali ikiwemo
kamati ya fedha ,
pamoja na dawa ili
kuweza kubadilisha na kumaliza matatizo ambayo yamekuwa sugu hususani dawa ambalo
limekuwa kama wimbo wa taifa .
Wapo watu wajanja wanaofanya
dawa hizi zisifike kwa wagonjwa, utafiti umefanywa na nyinyi wenyewe, kamati ya dawa iundwe sio ile kubwa hii ni
ndogo ya kuhakikisha pale dirishani kwa mfamasia ni wangapi wamepata dawa zote,
wangapi wamekosa , lakini katika mifumo yetu ya fedha viko vitengo
vinatumia vifaa tiba vibaya rasilimali lakini ukiangalia wateja wangapi wamechangia
hakuna takwimu , tunataka kamati ya fedha itakayosimamia hayo.
Aliongeza
kutaja kamati nyingine ya damu itakayosisimamia uchangiaji wa damu
Mfumo wa damu salama
wananchi wanalalamika watu wanakosa
damu wanashurutishwa wachangie kwanza ndipo wapewe damu nimefika kwenye vituo
malalamiko yapo sahihi ni kikundi cha watu wachache wajanja wajanja , lakini wananchi
suala lingine na ninyi hamchangii damu nimeona hapa kuanzia julai mpaka septemba asilimia 27 % ya chupa zilizotakiwa kupatikana asilimi ni
ndogo sana lakini je tunashirikishaje mifumo ya wadau waliopo kwenye mkoa huu
ili waweze kuhamasisha wananchi kuchagia damu . kamati ya damu iuundwe ili
kusimamia hili.
Akizungmza
kwa niaba ya
mkuu wa mkoa
, Mkuu wa wilaya Mhandisi Pascas Mulagiri
amethibitisha kupokea shilingi bilioni 5.9 ambapo ameanisha kuwa fedha hizo
zinatumika katika ujenzi wa hospitali ya rufaa ya mkoa
“Sisi ni miongoni mwa
wanufaika wakubwa mipango ya afya singida tayari tumepokea bilioni 5.9 katika uendelezaji wa hospitali ya
rufaa ya mkoa singida na ujenzi wake
unaendelea na haya lakini tuna pesa Bilioni 5.3 kwaajili ya ujenzi wa majengo
mbalimbali ambayo yataanza hivi karibuni
haya yakifanyika itakuwa ni mapinduzi makubwa sana katika sekta ya afya
hospitali yetu inakuwa ya rufaa na ukiwa
na hospitali hiyo itasaidia kuwa huduma nzuri na kuwa madaktari bingwa” .
alisema Mhandisi Mulagiri
Kuhusu
changamoto ambayo waliyokuwa nayo halmashauri kukosa hospitali ya wilaya mkuu
huyo wa wilaya wa Singida Mhandisi Mulagiri amesema walikosa huduma nyingi ikiwemo
madaktari bingwa ngazi ya wilaya.
Suala la kutokuwepo
kwa hospitali ya wilaya lilituaathiri
kwa kiasi Fulani ukiangalia katika sekta ya aafya mgawanyo wa huduma za
afya , madawa , wahudumu waafya unaendana na kituo hivyo tulikuwa tunakosa
mgawanyo wa dawa na huduma zingine hivyo
ujio wa hii nafasi ya kutimia majengo ya hospitali ya general utawasogezea
wananchi huduma kuwa karibu.
Mkandarasi
wa hospitali ya rufaa ya mkoa kutoka kambuni
ya MCB Justine Kyando amesema kwa sasa ujenzi huo umefikia asilimia 70 huku
akitoa makadirio ya kumalizika kwa ujenzi huo ili hospitali inaze kuanza
kutumika
“Tunashukuru ujio wa
mheshimiwa waziri . kwa sasa tumefikia asilimia 70 , kwa sahivi kwa sababu wanataka
kutuongezea mkataba kumaliza hadi
ghorofa tunaweza inaweza kutumia mwaka
mmoja na nusu kwa maana hadi mwaka 2023 tunaweza kumaliza ianze kutumika.”