METDO Tanzania

METDO Tanzania
Showing posts with label Habari za kimataifa. Show all posts
Showing posts with label Habari za kimataifa. Show all posts

Friday, February 6, 2026

BALOZI MWAMWETA NA MHE. MTAKA WASAKA SOKO LA PARACHICHI UJERUMANI

 

 Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Mhe. Hassani Iddi Mwamweta anaongoza ujumbe wa wakulima na wafanyabiashara kutoka Tanzania unaoshiriki Maonesho ya Kimataifa ya Matunda na Mbogamboga ya Fruit Logistica 2026 yanayofanyika Berlin kuanzia Februari 03 hadi 06, 2026.

Ujumbe huo unajumuisha Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA), Bw. Saleh Saad Mohamed unatumia maenesho hayo kupata fursa ya kutanua masoko kwa kuongeza masoko mapya, kuongeza mtandao wa wafanyabiashara na kujifunza maarifa mapya kuhusu kilimo-biashara.

Kampuni zaidi ya 40 kutoka Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi za TAHA, Mamlaka ya Udhibiti Nafaka na Mazao mchanganyika (COPRA) na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) wameshiriki Maonesho hayo ambayo yamehudhuriwa na kampuni zaidi ya 2600 kutoka nchi 151 duniani.

Fruits Logistica ni Maonesho ya Kimataifa ya Matunda na Mbogamboga ambayo huwaleta pamoja wakulima, wasambazaji, wanunuzi, wasafirishaji na wadau mbalimbali katika mnyororo wa usambazaji wa matunda na mbogamboga kutoka duniani kote.









Share:

Tuesday, December 16, 2025

MRADI WA SHILINGI MILIONI 120 WA VYOO VYA KISASA KUBORESHA USAFI NA AFYA MINADA YA BAHI NA KIGWE

 

 Na Meleka Kulwa – Dodoma

‎Mkurugenzi wa Miradi wa Habitat for Humanity Tanzania, John Massenza, amesema ujenzi wa vyumba vya vyoo vya kisasa katika minada ya Bahi na Kigwe utakapokamilika, utaimarisha mazingira ya biashara, afya, na usafi kwa wafanyabiashara pamoja na wananchi wanaotumia minada hiyo wilayani Bahi, jijini Dodoma.

‎Ziara ya kukagua na kukabidhi maeneo ya ujenzi ilifanyika Desemba 16, 2025, ambapo John Massenza amekabidhi rasmi maeneo ya miradi hiyo kwa wahandisi watakaotekeleza ujenzi wa vyumba vya vyoo katika minada ya Bahi na Kigwe.

‎Amesema kuwa katika mradi huo, kutajengwa majengo ya vyoo pamoja na miundombinu rafiki kwa wanawake, ikiwemo jengo maalumu litakalowawezesha wakina mama kujisitiri wanapokuwa na mahitaji maalumu.

‎Aidha, amesema kuwa katika minada ya Bahi na Kigwe kutajengwa jumla ya vyumba 26 vya vyoo, vikiwemo vyumba 10 kwa wanaume na 16 kwa wanawake, pamoja na tanki la maji kwa kila mradi. Miradi hiyo pia itajumuisha chumba maalumu cha mahitaji ya wanawake, bafu, chumba cha wakina mama wanaonyonyesha, pamoja na ofisi ya wasimamizi wa huduma.

‎Amebainisha pia kuwa vyumba viwili kwa kila mradi vitajengwa kwa ajili ya watu wenye ulemavu katika minada ya Bahi na Kigwe.

‎Aidha, amebainisha kuwa mradi wa ujenzi wa vyumba vya vyoo katika Mnada wa Bahi utagharimu shilingi milioni 60, huku mradi wa Mnada wa Kigwe ukigharimu shilingi milioni 60 pia. Miradi hiyo inatarajiwa kunufaisha zaidi ya watu 4,000 pindi itakapokamilika.

‎Katika mpango wa uendeshaji wa huduma hizo, amesema kuwa watumiaji wa vyoo watalipia huduma hiyo kwa lengo la kugharamia matengenezo, uendeshaji wa mradi pamoja na kuboresha makazi ya wananchi na kuinua vipato vyao.

‎Amebainisha kuwa utekelezaji wa miradi hiyo unalenga kuboresha afya na ustawi wa jamii, kuongeza kipato, na kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja kupitia mazingira bora ya biashara na huduma.‎

‎Habitat for Humanity inafanya kazi katika nchi 70 duniani, huku makao makuu yake yakiwa nchini Marekani. Aidha, Massenza amesema kuwa mradi huo ni sehemu ya jitihada za taasisi hiyo katika kuboresha huduma za vyoo na usafi wa mazingira katika maeneo ya minada na jamii kwa ujumla.

‎Katika ziara hiyo, Mkurugenzi wa Habitat for Humanity Tanzania, John Massenza, aliambatana na viongozi wa serikali ya kijiji na mtaa pamoja na maafisa mazingira kutoka Wilaya ya Bahi.

‎Awali, mhandisi wa mradi alisema kuwa tanki la maji litakuwa na ujazo wa lita 3,000, kwa Kila tank litakalokuwepo kwenye miradi hio, huku akibainisha kuwa ujenzi wa majengo hayo ukitarajiwa kuchukua wiki 8 hadi 10, na kwamba mradi mzima unatarajiwa kukamilika ndani ya siku 90.


















Share:

Friday, December 12, 2025

SERIKALI YAJIDHATITI KUIMARISHA USTAWI WA JAMII.



 Na Jackline Minja MJJWM , Dodoma

Serikali ya Awamu ya Sita, inaendelea kuweka kipaumbele katika ajenda ya ustawi na mifumo ya ulinzi wa mtoto, kuendeleza huduma za malezi mbadala, usimamizi wa Makao ya Watoto nchini ili kuhakikisha yanatoa huduma kwa viwango vinavyotakiwa.


Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi wakati wa ziara ya kutembelea Makao ya Watoto ya Taifa Kikombo Jijini Dodoma na kujionea huduma zinazotolewa katika Makao hayo.


Mhe. Maryprisca amesema Makao ya Taifa ya Kikombo ni mfano wa Taasisi ya Serikali inayotekeleza majukumu hayo kwa weledi, upendo na dhamira ya dhati.


“Nimetembelea miradi, miundombinu na kupokea taarifa ya mafanikio, changamoto na maeneo yanayohitaji kuimarishwa, nafurahishwa kuona jitihada kubwa zinazofanywa katika kutoa huduma ya Elimu, Afya, Lishe, ushauri nasaha pamoja na malezi kwa Watoto napenda kuwahakikishia kuwa Wizara itahakikisha Makao haya yanawezeshwa ipasavyo”. amesema Mhe. Maryprisca.


Aidha Mhe. Maryprisca ametoa rai kwa wadau wa maendeleo, mashirika ya kiraia, sekta binafsi na jamii kuendelea kushirikiana na Wizara kwa kuwapa watoto fursa sawa za maendeleo kama ilivyo kwa watoto wengine wote wa Tanzania.


“Niwaombe Mashirika, wadau wa maendeleo tuendelee kuiunga mkono Serikali katika kuendeleza makazi ya watoto ili wawe na huduma nzuri na wasijione wanyonge na niwaambie kuwa ninyi ni watu muhimu, mnapendwa na Taifa linawahitaji, msipoteze matumaini, someni kwa bidii, zingatieni maadili, muwe na nidhamu na mtumie fursa mnazopata ili mkafikie ndoto zenu."

amesema Mhe Maryprisca


Katika hatua nyingine Mhe. Maryprisca ameupongeza Uongozi wa Makao ya Taifa ya Kikombo kwa kazi wanayoifanya na kuwataka kuendeleza ushirikiano ili kuhakikisha kuwa kila mtoto analelewa katika mazingira salama, yenye upendo na yenye kumjenga.


Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Wakili Amon Mpanju amesema watumishi wa Makao hayo wana weledi na uwezo mkubwa wa kutambua uwezo wa watoto licha ya changamoto wanazokuja nazo watoto katika makazi hayo.


“Hawa watumishi unaowona hapa wanauwezo wa kukaa nao, kuongea nao kwa mbinu tofauti ndio maana nasema hawa sio watu wakawaida hata mimi wakiniangalia wanasema hapo hauko sawa, lakini ni miongoni mwa watu walioaminiwa na Serikali ambao watatusaidia kukiendeleza Makao haya”. amesema Wakili Mpanju.


Awali akisoma taarifa ya huduma zinazotolewa katika makao ya Taifa ya watoto kikombo Afisa Ustawi wa Jamii Anord Fyataga amesema hadi sasa kituo kimepata mafanikio mengi ikiwemo kuimarika kwa huduma za ushauri na unasihi ambapo kila mtoto anapata ushauri wa moja kwa moja au wa makundi ,kuunganisha watoto 20 na familia zao, kuboreshwa kwa huduma za elimu ndani na nje ya makao ambapo wastani wa ufaulu wa watoto kwa shule za msingi na sekondari umeongezeka kwa asilimia mbili (2%) pamoja na kuwajengea ujuzi watoto 40 katika ujifunzaji wa stadi mbalimbali za maisha makaoni kama ushonaji wa nguo kwa kutumia cherehani.





Share:

WAZIRI WA ARDHI AWAASA WAHITIMU ARIMO KUJIEPUSHA NA MATENDO MAOVU


Na Munir Shemweta, WANMM MOROGORO

 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amewaasa wahitimu wa Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) kujiepusha na matendo maovu na elimu na maarifa waliyopata yawe tunu na faida kwa Taifa.


Mhe. Dkt Akwilapo ametoa wito huo tarehe 12 Desemba 2025 wakati wa mahafali ya 44 ya Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) yaliyofanyika mkoani Morogoro ambapo jumla ya wahitimu 450 wa fani za Jiomatikia (Upimaji Ardhi), Upangaji Miji na Vijiji na Mifumo ya Taarifa za Kijiografia (GIS) walitunukiwa Astashada na Stashahada katika fani hizo.


Mhe. Dkt Akwilapo amewataka wahitimu hao kukumbuka kuwa utii, nidhamu na tabia njema ni silaha itakayowafanya wapendwe mahali popote.


‘’Tukiwa hapa Morogoro tunakumbuka maneno yaliyoimbwa na mwanamuziki wa hapa hayati Mbaraka Mwinshehe na bendi yake ya Okestra Volcano; alisema “Heshima Kijana tanguliza kwanza mbele, ujeuri mbaya; uzuri si hoja tabia njema ni silaha utapendwa popote” mwisho wa kunukuu, alisema Mhe. Dkt Akwilapo.


Amewataka vijana kutodanganyika na maneno ya eti kuna watu wanaitwa Gen Z ambapo alieleza kuwa, hizo ni propaganda za kujenga hofu na kufifisha juhudi za nchi maskini kujitafutia maendeleo.


“Msidanganywe kuwa eti nyie ni kizazi cha vijana wasio na nidhamu, wapenda fujo, wasiosikiliza wazee wao, viongozi wao, chenye kujiamulia mambo yao bila kufuata sheria, taratibu, miongozo na tamaduni zetu; na mambo mengine ya hovyo’’ amesisitiza Mhe. Dkt Akwilapo.


Kwa mujibu wa Waziri huyo wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, inasikitisha na kushangaza kuona vijana wa Kitanzania wanasikiliza maelekezo ya watu ambao hawaishi Tanzania na wala hawajawahi kuwaona na kupuuza maelekezo ya Viongozi wao na hata wazazi wao ambao wamewalea mpaka hapo walipoifikia.


Amesema, kuhitimu masomo kunatakiwa kuendane na uzalendo waliojengewa wa kuipenda Tanzania na kusisitiza kuwa waithamini nchi yao.


Mhe. Dkt Akwilapo amewataka kutumia utaalamu walioupata kwa weledi, uadilifu na kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo na kuepuka vitendo vinavyoenda kuhatarisha amani.


Vile vile amewataka kuendelea kujifunza kwani elimu ni bahari, haina mwisho na kuwataka wanaobaki chuoni kuongeza bidii katika masomo, nidhamu na kutunza amani na umoja kwani kesho yao inajengwa na maamuzi ya leo.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Bw. Musa Ramadhani Kilakala akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bw. Adam Malima amesema, migogoro ya ardhi imepungua mkoani humo hasa pale wizara ya ardhi ilipoanzisha Kliniki za Ardhi ambazo amezieleza zimesaidia kwa kiasi kikubwa kuwafikia wananchi katika maeneo yao.

Akitoa taarifa kwa Mgeni Rasmi, Mkuu wa Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) Charles Saguda amesema chuo hicho kina Mpango Kabambe wa Miaka 20 (2023-2043) unaolenga kuboresha mazingira ya kujifunza na kujifunzia na utendaji wa chuo katika kuwaandaa wataalamu wa sekta ya ardhi.

“Mpango kabambe huu unalenga kuongeza udahili wa wana chuo kutoka 660 hadi 5000, kuongeza watumishi kutoka 58 hadi 310 kuongeza program za mafunzo ya wanafunzi kutoka 2 hadi 7 pamoja na kujenga kampasi mpya katika eneo Mlima Kola mkoani Morogoro’’. Amesema Bw. Saguda.





Share:

Sunday, November 28, 2021

SERIKALI YATOA SHILLINGI BILIONI 5.9 UJENZI HOSPITALI YA RUFAA MKOA WA SINGIDA UJENZI WAFIKIA ASILIMIA 70

 Na Hamis Hussein - Singida

Serikali imetoa shilling bilioni 5.9 kwaajili ya kuendeleza ujenzi wa majengo mapya ya  hospitali ya rufaa ya mkoa  wa Singida ambayo itarahisisha huduma mbalimbali afya  ikiwemo upasuaji , tiba za kibingwa na  kupunguza gharama za matibabu kwa  wananchi kufuata huduma hizo  hospitali zingine za mbali  kama  Benjamini Dodoma , au muhimbili.



Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dr Doroth Gwajima ametembelea kukagua ujenzi huo akiwa kwenye  ziara ya kikazi  na kuridhishwa ujenzi huyo baada ya  kuona umefikia  asilimia 70  ikiwa ni  awamu ya kwanza ya fedha zilizotengwa .

DR. Gwajima alisema kukamilika kwa hospitali hiyo kutasaidia  kuruhusu wodi za hospitali ya rufaa ambayo majengo yake  yameshachakaa kuhamishiwa kwenye majengo mapya  ambayo yanajengwa  eneo la mandewa  pamoja na  kurahisisha huduma za afya kwa jamii.

“Kutoka singida nimekuja ziara fupi kuangalia maendeleo ya ujenzi wa hospitali mpya . iliyopo sasahivi ile hospitali iliyopo katikati ya mji imebanwa majengo yake yamepitwa na wakati   , umefika wakati wa kuongeza  kasi ili huduma za rufaa zihamie hospitali mpya ya mandewa  ambayo ni ya kisasa. Serikali  haiko nyuma imeshatenga  na kuleta shilingi bilioni 5.9 . Jengo lote linavyooneka hapa  ni kubwa  kuna sehemu ya upasuaji , maabara na wodi mbalimbali . hii itaruhusu wodi za kule zilizobanana kuhamia huku na  majengo ya hospitali ile yatumike na halmashauri  na hospitali hii itakapo kamilika itatoa nafuu kwa hospitali ya Benjamini mkapa pamoja na gharama za kwenda kutibiwa mbali ”. amesema Dr. Doroth Gwajima.


Wakati akikagua ujenzi wa majengo mapya ya hospitali Waziri Doroth Gwajima ametoa maagizo kwa viongozi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa singida pamoja na watendaji wengine kutoka serikalini kuundwa kwa kamati mbalimbali ikiwemo kamati ya fedha ,  pamoja na dawa ili kuweza kubadilisha na kumaliza matatizo ambayo yamekuwa sugu hususani dawa ambalo limekuwa kama wimbo wa taifa .

Wapo watu wajanja wanaofanya dawa hizi zisifike kwa wagonjwa, utafiti umefanywa  na nyinyi wenyewe, kamati ya dawa iundwe  sio ile kubwa  hii  ni ndogo ya kuhakikisha pale dirishani kwa mfamasia ni wangapi wamepata dawa zote, wangapi wamekosa , lakini katika mifumo yetu ya fedha viko vitengo vinatumia   vifaa tiba vibaya rasilimali  lakini ukiangalia wateja wangapi wamechangia hakuna takwimu , tunataka kamati ya fedha itakayosimamia hayo.

Aliongeza kutaja kamati nyingine ya damu itakayosisimamia uchangiaji wa damu   

Mfumo wa damu salama wananchi wanalalamika   watu wanakosa damu wanashurutishwa wachangie kwanza ndipo wapewe damu nimefika kwenye vituo malalamiko yapo sahihi ni kikundi cha watu wachache wajanja wajanja , lakini wananchi suala lingine  na ninyi hamchangii damu  nimeona hapa kuanzia julai mpaka septemba   asilimia 27 %  ya chupa zilizotakiwa kupatikana asilimi ni ndogo sana lakini je tunashirikishaje mifumo ya wadau waliopo kwenye mkoa huu ili waweze kuhamasisha wananchi kuchagia damu . kamati ya damu iuundwe ili kusimamia hili.




Akizungmza kwa niaba ya  mkuu wa mkoa  , Mkuu wa wilaya Mhandisi Pascas Mulagiri amethibitisha kupokea shilingi bilioni 5.9 ambapo ameanisha kuwa fedha hizo zinatumika katika ujenzi wa hospitali ya rufaa ya mkoa

“Sisi ni miongoni mwa wanufaika wakubwa mipango ya afya singida tayari tumepokea  bilioni 5.9 katika uendelezaji wa hospitali ya rufaa ya mkoa singida  na ujenzi wake unaendelea na haya  lakini tuna pesa  Bilioni 5.3 kwaajili ya ujenzi wa majengo mbalimbali ambayo yataanza hivi karibuni  haya yakifanyika itakuwa ni mapinduzi makubwa sana katika sekta ya afya hospitali yetu inakuwa  ya rufaa na ukiwa na hospitali hiyo itasaidia kuwa huduma nzuri na kuwa madaktari bingwa” . alisema Mhandisi Mulagiri

Kuhusu changamoto ambayo waliyokuwa nayo halmashauri kukosa hospitali ya wilaya mkuu huyo wa wilaya wa Singida Mhandisi Mulagiri amesema walikosa huduma nyingi ikiwemo madaktari bingwa ngazi ya wilaya.

Suala la kutokuwepo kwa hospitali ya wilaya lilituaathiri  kwa kiasi Fulani ukiangalia katika sekta ya aafya mgawanyo wa huduma za afya , madawa , wahudumu waafya unaendana na kituo hivyo tulikuwa tunakosa mgawanyo wa dawa  na huduma zingine hivyo ujio wa hii nafasi ya kutimia majengo ya hospitali ya general utawasogezea wananchi huduma kuwa karibu.

Mkandarasi wa hospitali ya rufaa ya mkoa  kutoka kambuni ya MCB Justine Kyando amesema kwa sasa ujenzi huo umefikia asilimia 70 huku akitoa makadirio ya kumalizika kwa ujenzi huo ili hospitali inaze kuanza kutumika

“Tunashukuru ujio wa mheshimiwa waziri . kwa sasa tumefikia asilimia 70 , kwa sahivi kwa sababu wanataka kutuongezea mkataba  kumaliza hadi ghorofa  tunaweza inaweza kutumia mwaka mmoja na nusu kwa maana hadi mwaka 2023 tunaweza kumaliza ianze kutumika.”


Share:

Tuesday, August 23, 2016

ANC chabwagwa uchaguzi wa Meya Johannesburg Afrika Kusini



Democratic Alliance kwa sasa kinashikilia baadhi ya miji mikubwa nchini humo
Chama tawala nchini Afrika kusini ANC kimepoteza udhibiti katika jiji la Johannesburg ambapo meya mpya wa jiji hilo Herman Mashamba anatoka chama cha upinzani cha Democratic Alliance.
Chama cha ANC kipo madarakani tangu kipindi cha ubaguzi wa rangi nchini humo zaidi ya miaka 20.

Mashamba ameahidi kubadilisha utawala wa jiji.
ANC ilipoteza majimbo mengi katika uchaguzi wa mwezi uliopita lakini bado ni chama kikubwa na kikongwe nchini humo.
BBC
Share:

Saturday, August 20, 2016

UNICEF:watoto wasajiliwa zaidi jeshini Sudani Kusini


Baadhi ya watoto wanaotumikishwa kama wanajeshi kwenye maeneo ya vita

Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF,limeonya juu ya ongezeko la watoto wanaosajiliwa kujiunga na jeshi ili kupigana vita nchini Sudani kusini.

Akiongea baada ya kufanya ziara katika maeneo ya Bentiu na Juba nchini Sudan Kusini, mkurugenzi mkuu wa UNICEF Justin Forsyth, alisema kuwa kuna hofu kuwa huenda watoto zaidi wakaingizwa jeshini.
Share:

Watoto waingizwa kwenye jeshi Sudan Kusini


Pande zote kwenye mzozo nchini Sudan Kusini zimejihami vikali

Serikali ya Sudan Kusini imewaajiri watoto wavulana kama wanajeshi wakati huu inapojiandaa kwa mzozo mpya, kwa mujibu wa shirika la Associated Press.

Mwanasiasa mmoja mwenye ushawishi anaripotiwa kuongoza shughuli ya kuwaajiri watoto hao, wengine wakitajwa kuwa na umri wa hadi miaka 12 kutoka kijiji kimoja nchini humo.
Share:
Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com