METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, September 4, 2020

Kikao cha Kamati ya Uongozi


Mkurugenzi idara ya Mtangamano wa Biashara, Ally Gugu, akizungumza wakati wa kikao cha kamati ya uongozi, katikati ni Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Riziki Shemdoe na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Mwinyi Talib Haji, kikao kimefanyika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) jijini Dodoma. 


Katibu Mkuu, Prof. Riziki Shemdoe katika picha ya pamoja na wajumbe walioshiriki kikao cha kamati ya uongozi kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Riziki S. Shemdoe Leo tarehe 3 Septemba, 2020 ameongoza kikao cha Kamati ya Uongozi (Steering Committee) ya Uwezeshaji Biashara katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) jijini Dodoma.

Lengo la kikao hiki lilikuwa ni kujadili utekelezaji wa maelekezo ya mkutano wa kwanza wa kamati hiyo uliofanyika tarehe 13 Februari 2020.

Masuala yaliyojadiliwa na kuidhinishwa ni pamoja na hadidu za rejea (ToR) za kamati ya kitaifa ya uwezeshaji biashara, Maeneo ya kundi A, B na C ya mkataba wa uwezeshaji biashara wa Shirika la Biashara la Dunia (WTO TFA) ambayo yatawasilishwa sekretarieti ya WTO kabla ya tarehe 22 Septemba, 2020.

Utekelezaji wa masuala mengine ya biashara nje ya mkataba wa uwezeshaji biashara, utekelezaji wa  mpango mwelekeo (Roadmap) wa miaka mitano (2020/21 - 2024/2025) na mpango kazi (Action Plan) ya mwaka 2020/2021. Aidha, Kamati imetoa maelekezo ya maboresho ya Mfumo wa taarifa za ufanyaji biashara (National Trade Information Module) kabla ya kufanyiwa uzinduzi rasmi.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com