Serikali kupitia Ofisi ya Waziri
Mkuu, Sera, Uratibu na Uwekezaji imeingia Mkataba na Mfuko wa Kimataifa
wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) kwa kusaini Makubaliano ya Awali ya
Programu ya Kuendeleza Sekta ya Uvuvi na Uzalishaji wa Mbegu Bora za
Mazao ya Kilimo nchini.
Mkataba huo ulisainiwa na Katibu
Mkuu wa Ofisi hiyo anayeshughulikia masuala ya sera, uratibu na
uwekezaji,Dorothy Mwaluko na Mkurugenzi wa IFAD kwa Nchi za Tanzania na
Rwanda Bw. Francesco Rispoli hii leo Oktoba 11, 2019 katika Ofisi Waziri
Mkuu Jijini Dodoma.
Mkataba huo wa awali umelenga
kuhakikisha kunakuwa na ongezeko la uzalishaji wa mbegu bora za mazao na
samaki na kuendelea kuwa na tija katika sekta ya kilimo na uvuvi.
Akizungumza kabla ya utiaji
saini wa mkataba huo, Katibu Mkuu wa ofisi hiyo amesema kuwa hatua hiyo
ni mwendelezo wa maboresho mbalimbali yanayoendelea kufanyika ili
kuwafikia wananchi katika kujiletea maendeleo kwa kuzingatia mchango wa
sekta ya Kilimo na Uvuvi nchini.
“Leo tumetia saini mkataba wa
makubaliano ya awali na Mfuko wa Kimataifa wa maendeleo ya Kilimo,
tunamatarajio makubwa katika hatua hii na huu ni mwanzo mzuri utakao
leta tija kwa maendeleo yetu,”allisema Mwaluko
Aidha, Mkurugenzi wa Mfuko huo
IFAD, Francesco Rispoli ameutaka Mfuko huo kutekeleza makubaliano hayo
ya awali kwa ufanisi, ikiwa ni pamoja kuzingatia maeneo yote kama
yalivyoainishwa katika mkataba huo.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi
wa Maendeleleo ya Biashara kutoka Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) Bi.
Jackline Shayo alieeleza kuwa uwepo wa makubaliano hayo utaleta chachu
katika kuendeleza sekta ya kilimo na uvuvi kwa kuzingatia malengo ya
mkataba huo.
“Kipekee niipongeze Serikali kwa
hatua hii ya awali, matarajio ni makubwa hususan endapo Mfuko huu
utatekeleza malengo kama ilivyokusudiwa na itasaidia kuleta maendeleo
katika sekta ya kilimo kupitia uboreshwaji wa miundombinu ya uzalishaji
wa mbegu bora,”alisema Shayo.
0 comments:
Post a Comment