Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akisisitiza jambo wakati akiongea na
Watumishi wa Sekta ya Afya, katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili
bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya
Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambae pia ni Mwenyekiti wa
Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula
Baadhi ya Watumishi wa Sekta ya Afya ambao pia ni
Wanachama wa TUGHE Taifa wakishikana mikono huku wakiimba wimbo wa kuhamasisha
umoja na mshikamano, wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti
ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma.
Na WAMJW – Dodoma.
Watumishi watakiwa kudumisha upendo, umoja na
mshikamano katika mahala pa kazi na kufanya kazi kwa bidii ili kutoa huduma
iliyo bora.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile alipokuwa akizungumza na
watumishi wa Sekta ya afya wakati wa ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi
lililofanyika jijini hapa
Dkt. Ndugulile amesema anaamini kuwa Wizara ya Afya
itafika mbali zaidi ikiwa watumishi watafanya kazi kwa bidii kwa kuzingatia
maadili ya utumishi wa umma na kuheshimiana bila kujali utofauti wa vyeo baina
ya watumishi.
“Kila mmoja amuheshimu mwenzake kwa sababu ana mchango
katika haya yote tunayoyafanya na tunategemeana sana kwenye kazi zetu za kila
siku” amesema Dkt. Ndugulile.
Aidha, Dkt. Ndugulile amewataka watumishi kuziheshimu
nafasi za uongozi walizonazo sasa kwa kuzienzi na kuhakikisha wanafanya kazi
ili kuthibitisha kuwa kweli wanastahili kuwa kwenye nafasi hizo.
“Bado kuna watumishi wengine hawajajitafakari katika
nafasi zao, lugha tunazozitoa, kutojituma, tuache kufanya kazi kwa mazoea”
alisema Dkt. Ndugulile.
Awali akizungumza na wajumbe wa mkutano, Mwenyekiti wa
Baraza hilo ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Zainab Chaula
amesisitiza watumishi kufanya kazi kwa umoja na kujitolea ili wote kwa pamoja
kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Katika Mkutano huo wajumbe walipitia na kujadili
masuala kadha wa kadha kuhusiana na Wizara ya Afya ikiwemo bajeti ya Wizara,
mabadiliko ya sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii, Sera ya Afya, Bima ya Afya
pamoja na masuala ya utendaji ndani na nje ya Wizara.
Mwisho
0 comments:
Post a Comment