METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, December 23, 2018

TGNP YAJIVUNIA MAFANIKIO WALIYOYAPATA KUPITIA MIRADI WANAYOSIMAMIA

Mtandao wa Jinsia nchini TGNP wajivunia  mafanikio waliyopata kupitia miradi  mbali mbali ilioanzishwa chini ya shirika hilo yenye lengo la ukombozi kwa mtoto wa kike dhidi ya ukatili wa kijinsia.
Baadhi ya washiriki wakiangalia picha mbalimbali za ukatili wa kijinsia pamoja na uwezeshaji wanawake na wasichana          katika tafrija iliyofanyika jana jijini Dar es salaam.


Akitoa ufafanuzi kupitia njia ya picha kwa washiriki wa semina hiyo mapema jana jijini Dar es salaam Afisa Program ya Harakati na Ujenzi wa Nguvu za Pamoja wa Mtandao huo Bi. Anna Sangai amesema kuwa miradi iliyoanzishwa kupitia Mtandao huo imeweza kumuokoa mtoto wa kike dhidi ya ukatili wa kijinsia ikiwemo ukeketaji na unyanyasaji katika jamii na kumfanya aweze kuishi kwa kujiamini.

“Kiukweli miradi hii imeweza kuokoa watoto wa kike dhidi ya kufanyiwa ukatili ukiwemo wa ndoa za utotoni, Ukeketaji na kudumazwa kiuchumi, hasa tukitazama  mradi wa Kipunguni ambao wanaharakati wameanzisha shughuli zao za kiuchumi na kumsaidia mtoto kuondokana na utegemezi”.alisema Sangai

Aidha,katika hafla hiyo iliyobeba kauli mbiu ya” AKEKETWI MTU, Mlinde mtoto wa kike dhidi ya ukatili ”baadhi ya viongozi wakiwemo  madiwani na wabunge kutoka sehemu mbali mbali walialikwa na kupata nafasi ya kutoa neno la kuwatia moyo wanaharakati kuwa wanaweza kufika wanapopataka kama watatia nia katika harakati zao.

“Niwatie moyo wanawake wenzangu mimi mwenyewe ni mmoja kati ya walionusulika kufanyiwa ukatili huo lakini nilisimama katika maamuzi ya kuhitaji kusoma na mpaka leo ni kiongozi japo nilipitia changamoto nyingi”.alisema Catheline Ruge,Mbunge viti maalumu mkoani mara.

Pia,Wanaharakati wamepongeza  jitihada ambazo TGNP mtandao unazifanya katika kuhakikisha wananchi wanapata elimu juu ya madhala yatokanayo na ukatili wa kijinsia kwa mtoto wa kike ikiwemo ukeketaji, Ndoa za Utotoni, Unyanyasaji na mengine huku wakihaidi kuendeleza harakati mpaka mtoto wa kike atapokombolewa kutoka katika ukatili huo.



Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao akitoa ufafanuzi kuhusiana na tafrija hiyo.

Baadhi ya wafanyakazi wa TGNP Mtandao wakijadili jambo fulani katika Maonesho ya picha za Mashujaa wa ukeketaji yaliyofanyika ofisi za shirika hilo mapema jana jijini Dar es salaam.

 Baadhi ya washiriki wakifuatilia tafrija.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com