Mbunge wa Jimbo la Vwawa Mkoani Songwe Mhe Japhet Hasunga ambaye
ni Waziri wa kilimo akizungumza kwenye kikao na baadhi ya walimu wa mkoa wa
Songwe kilichofanyika katika kata ya Vwawa tarehe 23 Disemba 2018. (Picha Zote
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Baadhi ya walimu Mkoani Songwe wakifatilia kwa makini maelezo ya
Mbunge wa Jimbo la Vwawa Mkoani Songwe Mhe Japhet Hasunga ambaye ni Waziri wa
kilimo wakati akizungumza kwenye kikao na baadhi ya walimu wa mkoa wa Songwe
kilichofanyika katika kata ya Vwawa tarehe 23 Disemba 2018
Mbunge wa Jimbo la Vwawa Mkoani Songwe Mhe Japhet Hasunga ambaye
ni Waziri wa kilimo akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye kikao na baadhi
ya walimu wa mkoa wa Songwe kilichofanyika katika kata ya Vwawa tarehe 23
Disemba 2018.
Mbunge wa Jimbo la Vwawa Mkoani Songwe Mhe Japhet Hasunga ambaye
ni Waziri wa kilimo akiwa katika picha ya pamoja na walimu wa mkoa wa Songwe
mara baada ya kikao kazi kilichofanyika katika kata ya Vwawa tarehe 23 Disemba
2018.
Na Mathias Canal, Songwe
Mbunge wa Jimbo la Vwawa Mkoani Songwe Mhe Japhet Hasunga ambaye
ni Waziri wa kilimo amewapongeza walimu kwa uzalendo wanaouonyesha katika
uwajibikaji wao katika kuhakikisha Taifa linasonga mbele kielimu.
Mhe Hasunga ametoa pongezi hizo wakati akizungumza kwenye kikao
kazi cha walimu wa shule za msingi na sekondari kutoka katika shule mbalimbali
za Mkoa wa Songwe kilichofanyika katika kata ya Vwawa.
Katika mkutano huo mbunge huyo ameridhia ombi la kuwa mlezi wa
walimu hao katika mkoa wa Songwe ambapo ameahidi kushirikiana kwa hali na mali
ili kutatua changamoto zinazowakabili walimu katika mkoa huo.
Alisema kuwa walimu wanapaswa kuheshimiwa kwani wanafanya kazi
kubwa ya kuongeza weledi kwa wanafunzi nchini ambapo wasomi hao ndio muhimili
wa Taifa.
Alisema pamoja na changamoto mbalimbali zinazowakumba walimu
ambazo zinaendelea kutafutiwa ufumbuzi na serikali lakini wameendelea
kutekeleza majukumu yao kwa weledi uliotukuka.
Katika kikao hicho walimu wameomba kutatuliwa changamoto sugu
ambazo ni pamoja na upandishaji wa madaraja, mapunjo ya mshahara, sambamba na
fedha za likizo na matibabu.
MWISHO.
0 comments:
Post a Comment