METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, February 2, 2018

NAIBU WAZIRI ULEGA AMMWAGIA SIFA MAVUNDE KWA KUBORESHA SEKTA YA ELIMU KATIKA JIMBO LA DODOMA MJINI

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akizungumza katika  hafla ya ugawaji wa kompyuta kwa Shule za Msingi na Sekondari 22 leo katika Viwanja vya Nyerere Square-Dodoma.

 Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akizungumza katika  hafla ya ugawaji wa kompyuta kwa Shule za Msingi na Sekondari 22 leo katika Viwanja vya Nyerere Square-Dodoma.
 Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akigawa kompyuta kwa Shule za Msingi na Sekondari 22 leo katika Viwanja vya Nyerere Square-Dodoma.
 Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde  na viongozi mbalimbali wakiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari 22 leo katika Viwanja vya Nyerere Square-Dodoma.
 Wanafunzi wakiwa katika hafla ya ugawaji wa kompyuta kwa Shule za Msingi na Sekondari 22 leo katika Viwanja vya Nyerere Square-Dodoma.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akikabidhi kompyuta kwa Shule za Msingi na Sekondari 22 leo katika Viwanja vya Nyerere Square-Dodoma.

Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akikabidhi kompyuta kwa Shule za Msingi na Sekondari 22 leo katika Viwanja vya Nyerere Square-Dodoma.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akikabidhi kompyuta kwa Shule za Msingi na Sekondari 22 leo katika Viwanja vya Nyerere Square-Dodoma akiwa na vion.ozi mbalimbali.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akikabidhi kompyuta kwa Shule za Msingi na Sekondari 22 leo katika Viwanja vya Nyerere Square-Dodoma akiwa na vion.ozi mbalimbali.

.............................................................................................................
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega amempongeza Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Anthony Mavunde ambaye pia ni Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu(Kazi,Vijana na Ajira) kwa kazi kubwa anayofanya ya kuwaletea wananchi maendeleo hasa katika kuboresha sekta ya Elimu jimboni humo.

Ulega ameyasema hayo leo wakati wa hafla ya ugawaji wa kompyuta kwa Shule za Msingi na Sekondari 22 leo katika Viwanja vya Nyerere Square-Dodoma.

Kompyuta hizo 22 zenye thamani ya Sh. Milioni 44 na zimetolewa na Mbunge Mavunde pamoja na wadau wa maendeleo katika kusaidia kuboresha sekta ya Elimu jimboni hapo.

Naibu Waziri Ulega amesema kwa sasa Dodoma ni Makao Makuu hivyo Mavunde  anapaswa kupongezwa kwa jitihada zake katika sekta ya elimu.
Ulega ambaye ni Mbunge wa Mkuranga amesema   kuna baadhi ya wazazi hawajawahamisha watoto wao Mkoani humo kutokana na uhaba wa shule  hivyo kupitia jitihada za Mbunge huyo shule zitaongezeka na idadi ya wanafunzi itakuwa kubwa.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mavunde ameahidi kuzipatia kompyuta shule zote 130 na kuahidi kuboresha miundombinu ya nishati katika shule zote ili wanafunzi wengi zaidi wapate nafasi ya kujifunza kwa kutumia teknolojia ikiwa ni muendelezo wa ugawaji wa vifaa vya kieletroniki katika mashule ambao ulitanguliwa na ugawaji wa vishkwambi (tablets)500 zenye thamani ya Sh.Bilioni 1.

Amesema Jimbo lake lina upungufu wa madarasa 1038 hivyo  kwa  kupitia mfuko wa Jimbo atatoa sh.milioni 55 ambazo zitatumika kufyatua matofali ili kupunguza upungufu huo.


Akimkaribisha Mgeni Rasmi,Kaimu Mkuu wa Wilaya wa Dodoma Mjini ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Kongwa Deogratias Ndejembi ameahidi kushirikiana na Mbunge kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya elimu ili kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata elimu bora katika mazingira rafiki.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com