METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, June 15, 2015

KUTOMALIZIKA KWA MAJENGO MENGI YA UMMA VIJIJINI KUNATOKANA NA UKOSEFU WA ELIMU YA USHIIKISHWAJI UMMA.



Na Denis Mkakala.

Wananchi wa kijiji cha Ibumila kata ya Mgama Halmashauri ya Iringa wameilalamikia seikali kwakutomaliza ujeenzi wa Zahanati ya kijiji hicho ikiwa wao wametimiza ufyatuaji tofali,kukusanya mchanga na kusogeza maji katika eneo lililoanza kujengwa zahanati hiyo tangu mwaka 2012.

 zahanati inayojengwa toka mwaka 2012.
 
Wakitoamalalamiko yao mbele ya Abraham Kimuli Afisa Uchechemuzi  wa TACOSODE wamesema kinamama wamekuwa wakizalia njiani wakati wakielekea kupata matibabu katika kituo cha afya cha ifunda ,hospitali ya Ipamba na hata katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa ikiwa nipamoja na baadhi ya akinamama ambao hupata madhara ya kubakiwa na baadhi ya vitu ndani ya miiliyao baada ya kujifungua.


mwenyekiti wa kijiji cha Ibumila RICHARD MHEMA Akiwa na wananchi katika zahanati inayoendelea kujengwa kijijini hapo.
 
Akitoaelimu baada ya malalamiko ya wananchi wa kijiji hicho  Afisa Uchehchezi Bw. Kimuli amesema jamii inapaswakutambua kuwa swala la ujenzi wa majengo ya umma wananchi wao wanatakiwa kusimamisha jingo mpaka kufikia eneo la bimu ambapo serikali itachukua jukumu la kuimalizia na kukamilisha ikiwapo na kuweka wauguzi na sio kuanzaujenzi wa jengo,hivyo ujenzi wa jengo la zahanati hiyo nijukumu lao wananchi hao na siswala la serikali.

TACOSODE ni mwamvuli wa mashirika yasiyo ya kiserikali wenye hadhi ya baaza hili pia lina hadhi ya kitaifa,Dira ya Tacosode kuwa asasi zenye uwezo wa kutetea haki za jamii na Dhamira kuwa na maendeleo endelevu kwa kujenga uwezo wa rasilimali watu,taasisis na wananchi kwa njia ya mafunzo,uwezeshaji wa rasilimali na mashiikiano kati ya wadau mbalimbali.
Nae diwani wa kata hiyo ya mgama Denis Lupala amesema ujenzi huo wa zahanati utakamilika mwezi wa 8 na kuiachia jukumu halmashauri katika kumaliazia jengo hilo ikiwa nipamoja na ujenzi wa barabara ambayo itatumiwa na wananchi wakijiji hicho katika kusafiisha mazao yao kupeleka sokoni.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com