METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, April 13, 2017

MAREKANI YAJISALIMISHA KWA CCM Z’BAR

Chama_Cha_Mapinduzi_Logo

NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR

SERIKALI ya Marekani imesema itaendelea kutoa misaada ya Kiuchumi, Ustawi wa jamii na kisiasa kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar   ili kuimarisha mahusiano ya nchi hizo  mbili.

Msimamo huo umeelezwa katika ziara ya Ujumbe wa Serikali ya Marekani uliotembelea Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar  kwa ajili ya kuzungumzia masuala ya sera za kiuchumi, kisiasa na kijamii huko Afisi Kuu Kisiwandui Unguja.

Marekani ambayo ni miongoni mwa Taifa kubwa lililoendelea kiuchumi, kijamii na kiulinzi hata katika masuala ya Kisiasa limesema kasi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ya awamu ya saba Zanzibar, linaishawishi taifa hilo kutoa misaada binafsi na inayopitia katika ngazi za kimataifa, ili kuenzi kwa vitendo juhudi hizo.

Hayo yameelezwa na Kiongozi wa Msafara huo ambaye ni Afisa wa kusimamia Masuala ya sera za kijamii na kisisa katika Ukanda wa Nchi za Afrika zilizomo katika jangwa la sahara, Bw. Gregory Simpkims wakati Akizungumza na Viongozi na Maafisa wa CCM waliongozwa na Naibu  Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Abdallah Juma Abdallah “ Mabodi”  hapo Kisiwandui Unguja.

Bw. Simpkims  alieleza kwamba Chama cha Mapinduzi (CCM)  kimekomaa kisiasa na kinaendelea kuimarika  tofauti na vyama vya kisiasa vya nchi nyingine , barani Afrika ambavyo baadhi yao vimeanza kupoteza nguvu na kuondolewa madarani na vyama vya upinzani.

“  Tuna nia ya kuisadia Zanzibar misaada mbali mbali ili iweze kukuza uchumi wake katika masuala ya kiuchumi, kijamii na kuimairisha mahusiano ya kibiashara.

Pia tunaamini kuwa vyama vya siasa vilivyopo Zanzibar  vitaendelea kulinda Amani ya Visiwa vya Zanzibar  bila kuruhusu ili viwe sehemu tulivu inayoshawishi kila taifa kufanya utalii na shughuli nyingine za kijamii.

Akitoa ufafanuzi  juu ya ugeni huo, Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho, Dkt. Abdallah Juma Abdallah “ Mabodi” alifafanua kwamba ujumbe huo pamoja na masuala mengine umesifu suala la serikali kuimarisha Amani na Utulivu wa nchi licha ya kuwepo kwa changamoto za kisiasa visiwani humo.

Pia ujumbe huo ulitaka kujua njia na sera zinazotumiwa na CCM kuendelea kuaminiwa na wananchi wa Tanzania na Zanzibar kwa ujumla, hali inayopekea kuimarika kwa uchumi wa nchi hiyo.

Alisema kwamba ujumbe huo ulitaka kujua mambo mbali mbali yakiwemo suala la Uchaguzi Mkuu uliopita wa mwaka 2015, siri ya kuimarika kwa CCM kisiasa na utekelezaji wa  Mipango(Programs) ya maendeleo na ustawi wa kiuchumi wa Taifa la  Marekani na sera za nchi za nje za taifa hilo kwa upande wa Zanzibar.

Alisema walizungumzia uimarishaji wa sera za kibiashara na kiuchumi ya Nchi za Afrika ambayo ni African Growth and Opportunity Act (AGOA), Mpango huo una Sheria inayorahisisha bidhaa kutoka Afrika ziingie katika soko la Marekani, na kueleza kuwa kwa sasa wapo tayari Zanzibar kunufaika na Mkakati huo ili Bidhaa zake zikauzwe katika soko hilo.

Dkt. Mabodi alisema ujumbe huo uliohoji kwa nini Taarifa ya wasimamizi wa kimataifa wa Uchaguzi (International Observers) wa mwaka 2015, ilikuwa tofauti na taarifa iliyotolewa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar  (ZEC).

Alifafanua kwamba jawabu la swala hilo Dkt. Mabodi alisema  kwamba CCM inaamini  na kuunga mkono taarifa na maelekezo ya Tume hiyo kwani ndio iliyokuwa ikisimamia shughuli za Uchaguzi toka awali na ilibainisha sababu kuu zaidi ya Tisa zilizosababisha Uchaguzi huo kufutwa, na hao waangalizi wa uchaguzi wa kimataifa walikuta mchakato huo ushaanza pia hawana uelewa wa kutoka juu ya siasa za Zanzibar.

Hata hivyo alisema kwamba pamoja na mambo mengine walitaka kujua kama ZEC wamewahi kutoa taarifa ya tathimini ya uchaguzi huo, na kuelezwa kuwa tayari imetolewa na kukabidhiwa rasmi kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein.

“ Wamezungumzia migogoro ya kisisa iliyozunga Zanzibar toka kumalizika kwea Uchaguzi Mkuu wa Octobar 25, 2015 nami nikawambia mizozo kama hiyo kisisa hasa katika mifumo ya kidemokrasia ni ya kawaida na kuwatolea mfano ambao hawakuupenda lakini sikuewa na namna ikabidi niwaulize kuwa katika Nchi yao toka kumalizika Uchaguzi Mkuu wa Rais Trump mbona mpaka leo, kuna shutuma na mizozo mbali mbali ikiwemo kuilaumu Urusi kuwa iliingilia masuala ya uchaguzi lakini pia Viongozi mbali mbali wamekuwa wakijiuzulu, na kuwahohoji ni Taifa gani limeingilia mambo yao ya siasa za ndani hawakuwa na jawabu rasmi la kunijibu”, alisema Dkt. Mabodi.

Sambamba na hayo Kiongozi huyo wa CCM Zanzibar, aliweka wazi kuwa alichojifunza kupitia mazungumzo hayo ni kuwa siasa na sera za kimataifa ni tofauti na Tanzania, kwani Nchi hizo zinatambua uhalisia wa siasa za Zanzibar licha ya kuwepo na baadhi ya wanasiasa wanaopotosha  na kuchochea vurugu.

Alisema pamoja na hayo ujumbe huo wa Ubalozi wa Marekani ulitaka Viongozi wa CCM kukaa meza moja na CUF kutafuta ufumbuzi wa mgogoro wa kisiasa uliozuka toka kufutwa kwa uchaguzi wa Octoba 2015, lakini Dkt. Mabodi akawafahamisha kwamba Chama chake kimeshamaliza Uchaguzi na Tayari Rais wa Zanzibar Dkt. Shein aliyepatikana kwa misingi ya kidemokrasia ataendelea kuongoza nchi hadi Uchaguzi wa 2020.

Alisema kuwa tayari baada ya Uchaguzi ulioharibika CCM kupitia viongozi wao waliitisha mazungumzo na CUF, lakini kabla ya kufikia makubaliano Maalim Seif Sharif Hamad alisusia mazungumzo hayo bila kutoa sababu za msingi.

Hata hivyo alisema Chama hicho kipo tayari kukaa na CUF kujadili utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020 pamoja na sera mbali mbali za SMZ, lakini sio kwa suala la Uchaguzi Mkuu uliopita.

Pia aliwambia wageni hao kuwa CCM imekuwa ikijitahidi kuwambia wananchi walinde Amani na Utulivu wa nchi na waendelee na shughuli za ujenzi wa Taifa kimaendeleo , lakini vyama vya Upinzani navyo vimekuwa vikipandikiza mbegu za chuki kwa kuwambia baadhi ya wananchi kwa  maeneo tofauti  wagome kushiriki katika harakati hizo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com