METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, March 22, 2017

BMT YATOA SOMO KWA WADAU WA MICHEZO

naddd
Na Carlos Nichombe

BARAZA la Michezo la Taifa(BMT) limewataka wadau wa michezo mbalimbali hapa nchini kuacha kasumba ya kuwategemea wadau kutoka jiji la Dar es Salaam katika kuongoza shughuli za vyama vyao.

Ofisa Habari wa Baraza hilo, Najaha Bakari amesema kumekuwa na tabia kwa baadhi ya wadau kuhisi kwamba watu wenye uwezo wa kushika nyadhifa za juu kwenye vyama vyao ni kutoka Dar es Salaam jambo ambalo linazidi kushusha maendeleo ya mpira hapa nchini.

Amesema kiongozi bora hatokani na mkoa anaotokea bali kinachotazamwa zaidi ni elimu pamoja na udhoefu ambao umewekwa na chama cha mchezo husika na sio kwamba wanakuwa wanaangalia eneo ambalo analotokea mdau anayetaka kugombea nafasi hizo.

Kauli hiyo ya Najaha imetolewa ikiwa ni siku chache zimepita tangu zoezi la uchukuaji fomu wa chama cha mchezo wa MASHUA ulipokamilika huku ikibainika idadi kubwa ya wagombea wa nyadhifa za juu wakitokea katika mkoa wa Dar es Salaam.

Amedai kitendo cha wadau wa mchezo wa mashua kutoka mikoa tofauti na Dar es Salaam kuogopa kugombea nyadhifa za juu kinaendeleza dhana potofu iliyojengeka kwa miaka mingi iliyopita.

“Ifike mahali wadau wa michezo hapa nchini tubadili mawazo yetu na tuone kwamba kila mtu mwenye sifa zilizoorodheshwa na vyama wakati wa uchaguzi anahaki ya kugombea nafasi yoyote ya uchaguzi pasipo kujali yeye ametokea mkoa gani na kama wadau hao watafanya hivyo ni imani yangu michezo itazidi kukua zaidi tofauti na sasa,” amesema Najaha.

Hata hivyo Najaha ameendelea kusikitishwa na mwenendo wa zoezi la uchukuaji fomu za kuwania nafasi mbalimbali za uongozi wa chama cha MASHUA ambalo limemalizika hivi karibuni na kudai hali ya ushindani katika uchaguzi huo inatarajiwa kuwa ni ndogo kuliko ilivyokuwa ikitarajiwa hapo awali
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com