METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, October 8, 2020

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA BARABARA ZA JUU UBUNGO FLYOVER JIJINI DAR ES SALAAM


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli wakati akikagua kazi za ujenzi wa barabara za Juu katika makutano ya Ubungo (Ubungo Flyover) jijini Dar es Salaam wakati akielekea Mbezi Louis kuweka jiwe la msingi Ujenzi wa Kituo Kikuu cha Kimataifa cha Mabasi ya Mikoani leo tarehe 08 Oktoba 2020.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia sakafu ya pili (gorofa ya pili) ya barabara za Juu katika makutano ya Ubungo (Ubungo Flyover) jijini Dar es Salaam wakati akielekea Mbezi Louis  kuweka jiwe la msingi Ujenzi wa Kituo Kikuu cha Kimataifa cha Mabasi ya Mikoani leo tarehe 08 Oktoba 2020.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwa katika picha na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Mhandisi Patrick Mfugale mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Juu katika Makutano ya Ubungo (Ubungo flyovers)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Mhandisi Patrick Mfugale wakati akiangalia mfano wa Ubungo Flyover utakavyokua mara baada ya kukamilika kwake.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia sehemu zilizokamilika katika barabara hizo za juu za Ubungo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi walipokuwa wakipita pembezoni mwa Daraja la Juu Ubungo flyover jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com