METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, September 23, 2016

Mbunge Mh. Zainab Nuhu Mwamwindi Atoa Msaada kwa shule ya Sekondari Mwembetogwa

Mh. Nuhu Mwamwindi akimkabidhi Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mwembetogwa, Bi Monica Kafumu mifuko ya saruji.

Msaada huo aliutoa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Matron wa Shule hiyo
Mbunge wa Viti maalum atokanaye na Jumuiya ya WAZAZI( C.C.M) Tanzania Bara, Mh. Zainab Nuhu Mwamwindi amesema kuwa jamii inahitaji kuhamasishwa na kukumbushwa wajibu muhimu wa kuunga mkono masuala muhimu yakiwemo yale yanayoweza kusaidia kusukuma mbele jamii ikiwemo elimu.
Aliyasema hayo wakati alikabidhi msaa da wa mifuko mia moja ya saruji kwa uongozi wa Shule ya Sekondari ya Mwembetogwa iliyoko katika Manispaa ya Iringa.
Aidha kwa kuguswa na mchango muhimu unaotolewa na walimu wa shule hiyo, Mh. Nuhu Mwamwindi alichangia papo hapo shilingi laki moja kwa ajili ya chai ya walimu shuleni hapo.
Mh.Mwamwindi akikagua mabweni ya hosteli ya wasichana iliyopo shuleni hapo.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com