METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, November 25, 2019

MKUU WA MKOA WA TANGA AKEMEA TABIA YA WAZAZI KUFUMBIA UKATILI DHIDI YA WATOTO


Mkuu wa Mkoa wa Tanga Bw. Martine Shigela akitoa hotuba kwa wadau wa kongomano la ukatili dhidi ya watoto leo Mkoani Tanga.
Badhi ya viongozi wa dini wa Mkoa wa Tanga wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Bw. Martine Shigela wakati wa kongomano la ukatili dhidi ya watoto leo Mkoani Tanga.
Badhi ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali za Mkoa wa Tanga wakifuatilia jambo wakati wa kongomano la ukatili dhidi ya watoto leo Mkoani Tanga.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Watoto kutoka Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii  Bw. Sebastian Kitiku akifafanua jambo kuhusu ukatili wa watoto mitandaoni wakati wa kongomano la ukatili dhidi ya watoto leo Mkoani Tanga.
……………..

Na mwandishi wetu TANGA.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Bw. Martine Shigela amekemea tabia ya Wazazi, Walezi pamoja na Jamii ya Mkoa wa Tanga kukumbatia vitendo vya ukatili dhidi ya watoto jambo ambalo linasababisha mkoa huo kuwa na takwimu za juu za vitendo vya ukatili kuliko mikoa mingine.


Mkoa wa Tanga kwa mujibu wa takwimu za jeshi la Polisi hapa Nchini unaongoza kwa vitendo vya ukatili dhidi ya watoto ndio maana Wizara ya Afya pamoja na wadau wameamua kuweka kongamano la vitendo vya ukatili dhidi ya watoto mkoani humo ili kujadiliana namna bora ya mkoa huo kuondokana na changamoto hiyo.


Mkuu wa Mkoa wa Tanga katika hotuba yake kwa wadau wa kongomano hilo amesema ni vitendo vya haibu kwa wakazi wa mkoa huo kuendelea kutajwa kuhusiana na ukatili dhidi ya watoto na hivyo kuwataka wadau wa kongamano hilo kuja na mkakati utakaowezesha mkoa huo kuweka mikakati ya kupambana na hatimaye kutokomeza kabisa ukatili dhidi ya watoto mkoani humo.


Aidha Mkurugenzi wa Watoto Wizara ya Afya   Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Bi.  Mwajuma Magwiza amesema kimsingi Kongamano hilo linafanyika Mkoani Tanga kutokana na Mkoa huo kuongoza kwa vitendo vya ukatili hapa Nchini akiongeza kuwa kongamano hilo linahusisha watoto, viongozi wadini na wazee mashuhuri wa mkoa huo ili kwa pamoja kutafuta namna bora ya kutokomeza vitendo hivyo.


Aidha Bi. Magwiza ameviambia vyombo vya habari kuwa Kongamano hilo lianaangazia changamoto ya ukatili dhidi ya watoto kama janga kubwa ambalo kimsingi halinabudi kuangaliwa upya kwa mustakabali wa ustawi wa maisha ya baadae ya mtoto.


Bi. Magwiza ameyataja maeneo manne ambayo Wizara yake na wadau watatotoa kwa ajili kuelimisha Kongamano hilo kuwa ni eneo la ukatili kwa ujumla wake, wajibu wazazi na walezi katika makuzi ya mtoto,ukatili wa watoto mtandaoni pamoja na umuhimu wa malezi na makuzi kwa ajili ya maendeleo ya  mtoto.


Wakati huo huo Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Watoto kutoka Wiazara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii  Bw. Sebastian Kitiku akifafanua zaidi kuhusu ukatili wa watoto mitandaoni ameonya wazazi na walezi hapa Nchini kuwa makini na watoto wakati wa matumizi ya vifaa vya kielektroniki kwani vifaa hivyo vinatumika katika kuendeleza vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.


Bw. Kitiku ameliambia kongamano hilo kuwa watoto ni weledi sana katika matumizi ya simu pamoja na television za kisasa na wanatumia muda mwingi katika vifaa hivyo akizitaja simu kuwa tishio kwani watoto wanapata ukatili wa kingono mtandaoni kupitia mawasiliano ya simu na kompyuta na kupelekea wengine kujiua baada ya kukosa usaidizi baada kufanyiwa ukatili na watu wasio wajua.


Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kila ifikapo leo tarehe 20 Novemba uungana na nchi nyingine Duniani kuadhimisha siku ya Kimataifa ya Haki za Mtoto pamoja na kusherehekea miaka 30 ya utekekelezaji wa Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto ndiyo dhana ya kongamano hili ambalo limefanyaika leo ili kutoa fursa kwa wadau wengi zaidi kushiriki kuadhimisha siku hii.


Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Mtoto ulipitishwa rasmi na nchi wanachama wa umoja huo mnamo tarehe 20 Novemba, 1989 sambamba na uanzishwaji wa Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto (Child Rights Convention) ambapo hadi sasa nchi 190 wanachama wa Umoja wa Mataifa ambazo zimetia saini na kuridhia mkataba huu.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com