Ikiwa
imebaki siku moja kabla ya kufanyika kwa Tamasha la 14 la jinsia, TGNP Mtandao
limemtaja Balozi Mama Getrude Mongela kuwa mgeni rasmi katika tamasha la 14
linalotarajiwa kuanza September 24 hadi
27, 2019.
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao. Lilian Lundi akitoa ufafanuzi wa jambo fulani ,mbele ya waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es salaam.
Haya
yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo Lilian Liundi wakati
akizungumza na waandishi wa habari Mapema leo Jijini Dar es Salaam.
Akifafanua
sababu za kumpa heshima Mama Mongela kuwa Mgeni Rasmi katika Tamasha hilo la
14, Liundi amesema kuna sababu nyingi za kufanya hivyo lakini kubwa ni harakati
zake alizozifanya hadi kufikia hatua za kuleta mageuzi ya kijinsia hapa Nchini.
“Kipekee Tanzania itakumbukwa katika historia kwa kuweka misingi ya usawa wa kijinsia na
haki za wanawake kwani katika mkutano wa Beijing Balozi Getrude mongela
aliibuka kidedea katika mkutano huo”. alisema Mkurugenzi
Ameongeza kuwa zaidi ya watu 1000 kutoka ndani na nje ya Tanzania wanatarajiwa kushiriki
Tamasha la mwaka huu, ambapo litaongozwa na kauli mbiu
inayosema 'Wanaharakati wa
Jinsia Mbioni Kubadilisha Dunia'
Lilian Liundi amesema washiriki wa tamasha
hilo watakuwa ni pamoja na wawakilishi wa asasi za kiraia kutoka ndani na nje
ya nchi, viongozi mbalimbali kutoka ngazi ya halmashauri na serikali
kuu, wanaharakati na wananchi wa kawaida.
Mkutano ukiendelea.
"Tunatarajia tamasha
la Jinsia la Mwaka huu litakuwa la kipekee kwani kitaifa na kidunia tumeanza
kusherehekea maadhimisho ya miaka 25 ya Azimio na Mpango kazi wa Beijing amabapo vitaenda sambamba na miaka 25 ya TGNP Mtandao".
Amesisitiza kuwa Tamasha hilo litaudhuliwa na wageni kutoka nchi kama Rwanda, Afrika kusini, Burundi, Swizland, Kenya, Uganda, Ghana na Zimbabwe na pia linatoa fursa kwa asasi
za kiraia zilizoshiriki katika mchakato wa Beijing kutakafari na kusherehekea
uwepo wa asasi hizo kwa zaidi ya miaka 25 ambapo azimio na mpango kazi Beijing
ndiyo iliyoweka misingii ya usawa wa kijinsia na haki za wanawake kidunia.
"Katika
kuendelea kuenzi na kuthamini mchango wa Mama Getrude Mongella,TGNP na Tapo la
Ukombozi,tumeamua kumchagua Balozi Mhe. Dr. Getrude Mongella aliyeongoza
mchakato wa Beijing na pia mchakato wa 'Kuileta Beijing Nyumbani' kuwa mgeni
rasmi wa Tamasha la Jinsia mwaka huu",alifafanua Liundi.
Alibainisha kuwa tamasha hilo litahusisha
mawasilisho,mijadala ya pamoja, maonesho na warsha, kusherekea mchango wa
mashujaa wanawake katika kufikia haki na usawa wa kijinsia.
Baadhi ya wanachama wa TGNP Mtandao wakiongea na waandishi wa habari.
Mkutano ukiendelea.
0 comments:
Post a Comment