METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, July 24, 2019

NDALICHAKO: NIMERIDHISHWA NA MAENDELEO YA UKARABATI WA SHULE ALIYOSOMA BABA WA TAIFA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa. Joyce Ndalichako amekagua maendeleo ya ukarabati na upanuzi wa shule ya msingi Mwisenge na kuridhishwa na kasi na ubora wa kazi ya ukarabati inayoendelea ambao umefikia asilimia 60.

 

Ukarabati wa Shule ya Mwisenge ambayo alisoma baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere ulianza kufanyika baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt John Pombe Joseph Magufuli kuitembelea na kuagiza ikarabatiwe na kujengewa ukuta.

 

Akizungumza akiwa katika ziara ya kukagua maendeleo mradi huo amesema ameridhishwa na kasi hiyo ya ujenzi huo ambao unahusisha ukarabati wa majengo ya kale, ukarabati wa madarasa, mabweni, ujenzi wa madarasa na mabweni mapya, ujenzi wa uzio kuzunguka shule hiyo, ukarabati wa mnara wa kumbukumbu pamoja na uboreshajii wa mazingira ya nje. 

 

Mradi huo unaogharimu kiasi cha sh Milioni 706 ambazo zimetolewa na Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia unatarajiwa ulianza Mwezi April na utakamilika na kukabidhiwa mwezi Septemba mwaka huu.

 

“Nimefurahishwa na hatua iliyofikiwa mpaka sasa na viwango vya ujenzi wa madarasa na mabweni nao ni imara, hata ujenzi wa ukuta unafanyika vizuri, kuta za mabweni ni ndefu na zitawafanya watoto wakiwa ndani wapate hewa vizuri”alisema Profesa Ndalichako.

 

Shule hiyo awali ilikuwa haina ukuta kabisa hali ambayo ilisababisha mazingira kuwa hatarishi kwa watoto hasa wenje ulemavu wa Ngozi. Ukuta huo umeshajengwa kuzunguka shule yote.

 

Katika hatua ingine ilionekana ukarabati wa baadhi ya majengo ya kihistoria katika shule hiyo ambapo moja ya jengo linalengwa kuwa zahanati itakayotumika kwa ajili ya wanafunzi umesimama. Akitoa taarifa ya ujenzi Mkuu wa Shule hiyo…. amesema majengo hayo yalisimama kutokana na Idara ya Mambo ya Kale kutowasilisha maoendejezo yao baafa ya kufanya tathmini.

 

Waziri Ndalichako amewataka watalaam hao kufika mara moja ili kutoa muongozo unaohitajika kuwezesha kukamilisha ukarabati wa majengo hayo kwa wakati.

 

“Ni vizuri ndugu zetu wa Mambo ya Kale wafike mara moja ili kutoa muongoza wa namna bora wa kufanya ukarabati wa majengo haya ya kihistoria yanapaswa kukarabatiwa kuwezesha ujenzi huo kukamilika mapema kuwezesha wanafunzi kupata fursa ya kuyatumia, kwani kuendelea kuchelewesha taarifa hiyo ni kukwamisha utekelezaji wa mradi.

 

Prof. Ndalichako amesema lengo la wizara ni kuona shule hiyo inakamilika mapema ili kutimiza maagizo aliyoyatoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jonh Pombe Magufuli ya kutaka shule hiyo ikarabatiwe iwe na hadhi ya Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere kuweka kumbukumbu nzuri ya shule aliyosoma.

 

Ndalichako ameshauri wajitahidi hiyo ikamilike mapema ikiwezekana kabla ya tarehe 14 Oktoba, siku ya kumbukumbu ya Baba wa Taifa ili iwe sehemu ya maadhimisho hayo.

 

Mapema Mkuu wa Wilaya ya Musoma , Dkt. Vicent Anney alimweleza waziri kuwa baadhi ya majengo hayajakamilika kutokana na kusimamishwa kwa ukarabati wa majengo hayo ya kihisitoria katika shule hiyo na Ofisi ya Mambo ya Kale yenye jukumu la kutoa muongozo wa namna gani ukarabati unapaswa kufanywa, ingawa toka kusimamishwa wataalam hao bado hawajafika kutoa maelekezo yeyote yale na tayari wameshawaandikia barua ya kuwakumbusha.

 

“Lengo letu ni kuhakikisha ifikapo Oktaba 30 ukarabati huu uwe yamekamilika kabisa, lakini changamoto iliyopo sasa ni kukwama kwa ukarabati wa baadhi ya majengo ya kihistoria ambayo wenzetu wa mambo ya kale waliagiza ukarabati wake usimame mpaka watakapofika na kutoa maelekezo ya namna gani ufanyike lakini mpaka sasa hakuna mtaalam yeyote aliyefika pamoja na kuwaandikia barua, Amesema Dkt. Anney.

 

Dkt. Anney ameishukuru wizara kwa kuipatia Wilaya ya Musoma fedha za kutekeleza miradi mbalimbali inayoendelea ikiwemo shilingi milioni 152 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za udhibiti ubora wa shule, ukarabati wa shule ya sekondari ya ufundi musoma ambayo imewekewa mitambo pamoja na vifaa vya kufundishia iliyogharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.2.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com