Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akitoa ufafanuzi kuhusu mafanikio ya changamoto za Wizara ya Kilimo wakati akizungumza kwenye kipindi cha Kumepambazuka kinachorushwa na Radio One Stereo Mikocheni Jijini Dar es salaam, leo tarehe 21 Machi 2019. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akihojiwa kwenye kipindi cha Kumepambazuka kinachorushwa na Radio One Stereo kuhusu mafanikio ya changamoto za Wizara ya Kilimo, Mikocheni Jijini Dar es salaam, leo tarehe 21 Machi 2019.
Na Mathias Canal, Wizara ya
Kilimo-Dar es salaam
Tangu serikali kutangaza mchakato wa
kuanza kuwasajili wakulima wote nchini kumekuwa na mapokeo tofauti tofauti kwa
wakulima na jamii kwa ujumla kwa kuogopa gharama za uandikishwaji.
Kufuatia sintofahamu hiyo serikali
imewatoa hofu wakulima nchini kuwa hakutakuwa na gharama ya aina yoyote
itakayomuhusisha mkulima wakati wote wa zoezi la usajili.
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga
(Mb) ameyasema hayo leo tarehe 21 Machi 2019 wakati akizungumza kwenye kipindi
cha Kumepambazuka kinachorushwa na Radio One Stereo Mikocheni Jijini Dar es
salaam kilichokuwa kinajadili changamoto na mafanikio ya Wizara ya Kilimo.
Ni hivi karibuni tu Waziri Hasunga aliziagiza
Bodi zote zilizoko chini ya Wizara ya Kilimo kuanza mara moja usajili wa
wakulima wa mazao yote na kuhakikisha kuwa zinawapa vitambulisho kwa ajili ya
kuwatambua na wanapofanyika kazi zao ili iwe rahisi kuwahuduma.
Akizungumza katika kipindi hicho cha Radio One
Waziri Hasunga alisema kuwa hatua hiyo inalenga kuwatambua na kuwasaidia
wakulima kuboresha kilimo chao ili waweze kupata huduma za uhakika kwa
ajili ya manufaa yao na Taifa kwa ujumla.
Alisema hatua hiyo inalenga kuwatambua
wakulima wote na maeneo ambayo wanalima ili kuwaondoa na kilimo cha kujikimu na
kuelekea katika kilimo cha kibiashara na kisasa.
“Lazima
tuanze kuwatambua wakulima wetu walipo, mashamba wanayolima na ukubwa wake na
mazao wanayolima na kiwango mazao ambacho wanatarajia kuzalisha ” alisisitiza. Na kuongeza kuwa ni lazima shughuli za kilimo zianzie kutambulika kama zilivyo taaluma
nyingine.
Alisema kukosekana kwa takwimu halisi za
wakulima , ukubwa wa mashamba yao na walipo kumesababisha kuwa vigumu huduma
muhimu kwa ajili ya kuboresha kilimo kuwafikia na kusababisha wapatiwe huduma
za kitaaalamiu ambao halizingani na mahitaji yao na wakati mwingine sio halisi.
Waziri hiyo wa Kilimo aliongeza kuwa nguvu
kubwa lazima ielekezwe katika kuwasaidia wakulima kulima cha kisasa kwa sababu
ndicho kinatoa ajira kubwa kwa Watanzania ambapo asilimia 65 ya wananchi
wamejiari katika kilimo na asilimia 8 wanashughulika na biashara inayotokana na
mazao ya kilimo.
Kadhalika, alisema kuwa kwa ujumla Wizara ya
Kilimo ina mikakati kabambe ya kuimarisha sekta ya mbegu, upatikanaji wa mbolea
kwa wakati, upatikanaji wa Viuatilifu sahihi sambamba na kutafuta masoko ya
mazao yote ya wakulima nchini.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment