Katibu mkuu wizara ya kilimo Mhandisi
Mathew Mtigumwe akimkabidhi Mkuu wa idara ya mafunzo ya kilimo huduma za ugani
na utafiti Dkt. Wilhelm Mafuru nakala ya mtaala uliozinduliwa katika kutano
uliofanyika kawenye hoteli ya Morena hivi karibuni
Katibu mkuu wizara ya kilimo Mhandisi
Mathew Mtigumwe akikata uteme kama ishara ya kuzindua mtaala wa kilimo katika
kutano uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Morena.
Na Bashiri Salum, Wizara ya Kilimo- Dodoma
Katibu
Mkuu Wizara ya Kilimo, Mhandisi Mathew
Mtigumwe leo tarehe 21 Machi,
2019 amezindua rasmi mtaala wa Kilimo uliohuishwa baada ya ule wa zamani uliofahamika kama
mtaala wa kilimo mseto kuboreshwa.
Akihutubia
mamia ya wataalamu kutoka Taasisi mbalimbali za Umma na Binafsi katika mkutano
uliofanyika kwenye Hoteli ya Morena
iliyopo Jiji la Dodoma, Mhandisi Mtigumwe amesema Mtaala huo ni matokeo
ya mahitaji ya soko la ajira (Labour Market Need Assessment)
yaliyofanywa na wataalamu waelekezi toka Chuo Kikuu Cha Iringa na kubaini umuhimu
kwa jamii.
Aidha
Katibu Mkuu huyo amebainisha kwamba
kulingana na maendeleo ya teknolojia kumekuwa na mahitaji makubwa ya wanafunzi
wa Vyuo vya Kilimo kuwezeshwa kubobea katika fani au taaluma zao (field of specialization) hivyo mtaala
huo umekuja wakati muafaka.
Aidha
Mtaala huo umehuishwa na kuingiza
taaluma na moduli mpya katika nyanja za Ushirika katika Kilimo, Hisabati katika
Kilimo, Mawasiliano, Mabadiliko ya tabianchi, Jinsia na Kilimo Endelevu; ili
kuwajengea uwezo na umahiri wahitimu katika sekta ya Kilimo (Agriculture
Production).
“Napenda kuwajulisha kuwa mtaala huu
umezingatia kanuni za NACTE, hivyo ninayo furaha kusema kuwa tumefanikiwa
kupata sio tu Mtaala Uliohuishwa bali pia ni Mtaala wenye moduli mpya sita
zilizojaza nafasi ya moduli za Mifugo” alisisitiza Mhandisi Mtigumwe
Hata hivyo Mhandisi Mathew Mtigumwe
alibainisha kwamba Mtaala mpya wa Kilimo (Agriculture Production) umehusisha moduli mpya zilizoingizwa katika tuzo ya taifa
ya ufundi daraja la nne NTA Level 4: mbinu za msingi za
mawasiliano Basic Communication Skills
na hisabati katika kilimo Basic
Mathematics in Agriculture; tuzo ya taifa ya ufundi daraja la tano NTA Level 5: menejimenti ya mazingira Environment Menagement na Kanuni bora za Ushirika
katika kilimo Principles of
Cooperatives in Agriculture; na tuzo ya taifa ya ufundi daraja la sita NTA
Level 6: kilimo hai/endelevu Organic
Farming na jinsia katika kilimo Gender in Agriculture.
Mtaala
uliohuishwa unalenga kutoa wagani tarajali wenye umahiri katika uzalishaji
mazao kwa tija na hivyo kuchangia katika sera ya uchumi wa viwanda alisisitiza
Mhandisi Mtigumwe.
Awali
Katibu Mkuu huyo alishukuru Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), Shirika la
LWR, Shirika la Kilimo Endelevu Tanzania (SAT), Baraza la Taifa la Elimu ya
ufundi NACTE, Wakala wa uzalishaji na usambazaji wa mbegu za kilimo (ASA), Taasis
ya Udhibiti wa Ubora wa Mbegu Tanznia (TOSCI), Halmashauri za Wilaya, Makampuni
Binafsi, Chuo Kikuu Cha Ushirika Moshi, Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam na Wizara ya Kilimo kwa kufanikisha upatikanaji wa mtaala huo.
Aidha,
Wakufunzi wetu wanahitaji kupata mbinu bora katika kutekeleza Mtaala mpya,
mazingira rafiki ya kujifunzia na kufundishia; haya ni maeneo mengine ya
mashirikiano, nasi tuko tayari kushirikiana na wadau mliopo na wadau wengine
alimalizia Mhandisi Mtigumwe.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment