Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda cha ubanguaji korosho cha Micronix kilichopo Wilayani Newala wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji mkoani Mtwara. Juzi 19 Machi 2019. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akitoa ufafanuzi kuhusu malipo ya wakulima wakati akizungumza na wananchi katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba wakati wa ziara ya kikazi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji mkoani Mtwara. Juzi 19 Machi 2019.
Wakazi wa Wilaya ya Tandahimba wakimlaki Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) mara baada ya kuzuru Wilayani humo akiwa katika ziara ya kikazi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji mkoani Mtwara. Juzi 19 Machi 2019.
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ikikagua kiwanda cha ubanguaji korosho cha Micronix kilichopo Wilayani Newala wakati wakiwa katika ziara ya kikazi katika mkoa wa Mtwara. Juzi 19 Machi 2019.
Sehemu ya wananchi Wilayani Newala wakifatilia mkutano wa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji wakati wakiwa katika ziara ya kikazi mkoani Mtwara. Juzi 19 Machi 2019.
Na Mathias Canal, Waziri wa
Kilimo-Mtwara
Mwezi Octoba mwaka 2018 Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli aliivunja rasmi
Bodi ya Korosho nchini huku Mkurugenzi Mkuu akiondoshwa pia kutokana na mwenendo hafifu kwenye biashara ya zao hilo.
Maamuzi hayo ya Rais yalitangazwa na
Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwa katika kikao na wakuu wa mikoa ya Lindi
na Mtwara ambapo kikao hicho kililenga kujadili hatua ya mgomo wa wakulima wa
korosho juu ya kushuka kwa bei ya zao hilo ukilinganisha na miaka miwili
iliyopita yaani 2016/2017 na 2017/2018.
Katika hatua nyingine Waziri wa
Kilimo Mhe Japhet Hasunga ametangaza maamuzi ya serikali kuwa imejipanga kuiunda
upya Bodi hiyo ya Korosho ili iendelee na majukumu yake ya kulisisimamia zao hilo kwa
ufanisi.
Mhe Hasunga ametangaza maamuzi hayo
ya serikali Tarehe 20 Machi 2019 wakati akijibu hoja za wakulima mbele ya
kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji wakati ikiwa katika ziara ya kikazi
kwenye Mkoa wa Lindi na Mtwara.
“Tumechakata vya kutosha kuhusu
mustakabali wa zao la Korosho na sasa tumedhamiria kama serikali kuiunda upya
Bodi ya Korosho ambayo itatekeleza majukumu yake kwa ufanisi mkubwa ili
kuongeza tija na uzalishaji wa zao hilo” Alisisitiza Mhe Waziri wa Kilimo
wakati akizungumza kwenye mkutano uliowakutanisha wakulima wa Korosho Wilayani
Tandahimba
Katika mkutano huo pia Waziri Hasunga alieleza kuwa mara baada ya kukamilika kwa malipo ya wakulima Machi 31 mwaka
huu Wizara ya Kilimo itapitia upya mfumo ulioutumika kuwalipa wakulima wa
korosho ili kubaini kama kuna mapungufu iyaweze kuboreshwa ama vinginevyo.
Alieleza kuwa serikali ina kusudio la
kuimarisha na kujenga viwanda vya kubangua korosho ili kuanzia msimu ujao
korosho zote za wakulima ziweze kubanguliwa nchini.
“Tukifanikiwa katika uwekezaji wa
viwanda na korosho zote tukazibangua wenyewe tutakuwa tumefanikiwa kuongeza
ajira za wananchi wetu sambamba na kuongeza thamani ya zao la korosho ndani na nje ya nchi” Alisema
Kadhalika, Waziri wa Kilimo ameeleza
kusudio la serikali kufanya mapitio ya sheria ya korosho kubaini mapungufu
yaliyopo na kuirekebisha upya.
Katika hatua nyingine Mhe Hasunga
aliieleza kamati hiyo kuwa wizara ya kilimo inaendelea na mkakati wake wa kuwasajili
wakulima wote nchini ili kujiimarisha, kuwatambua na kuongeza tija katika
kuwahudumia.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment