METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, January 3, 2018

JAFO,PROF.MAJI MAREFU WAUNGURUMA KAMPENI ZA UDIWANI KATA YA KWAGUNDA KOROGWE

Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo akimnadi Mgombea udiwani wa Kata ya Kwagunda(CCM) Saidi Athumani maarufu kwa jina la Moto.
Mbunge wa Korogwe Vijijini Stephen Ngonyani  akizungumza katika kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kwagunda
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo akiwa na viongozi mbalimbali katika kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kwagunda
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo akiwa na viongozi mbalimbali katika kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kwagunda
Umati wa wananchi waliokuwepo kwenye kampeni za udiwani kata ya kwagunda

KAMPENI za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kwagunda wilayani Korogwe zimeendelea kushika kasi ambapo leo Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo na Mbunge wa Korogwe vijijini Stephen Ngonyani maarufu kwa jina la Prof. Majimarefu wameunguruma kumnadi mgombea wa CCM  Saidi Athumani maarufu kwa jina la Moto.

Uchaguzi umetokana na aliyekuwa diwani wa kata hiyo kufariki dunia miezi michache iliyopita.

Katika kampeni hizo, Jafo ambaye pia ni Mbunge wa Kisarawe ndiye aliyekuwa mgeni rasmi akiwa na mwenyeji wake  Prof. Majimarefu wamewaeleza wananchi kwamba watumie fursa hiyo kuhakikisha januari 13 mwaka huu hawafanyi makosa wamemchague Saidi ili aweze kuwatumikia ipasavyo.

Wamewataka wananchi kukiamini chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwa chini ya Rais John Magufuli kimejipambanua kuwatumikia wananchi wanyonge na maskini.

Mkutano huo ulihudhuriwa na umati mkubwa wa wananchi huku CCM ikidhihirisha imejipanga kupata ushindi wa kishindo katika uchaguzi huo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com