Na Binagi Media Group
Novemba 14 kila mwaka Tanzania huungana na mataifa mbalimbali kuadhimisha Siku ya Kisukari Duniani ambapo pamoja na mambo mengine, lengo ni kutoa elimu kwa wananchi kuhusu ugonjwa wa kisukari ili kutambua namna ya kujiepusha na ugonjwa huo.
Katika kuadhimisha maadhimisho hayo mwaka huu yaliyofanyika jana, Chama cha Watoa Huduma za Afya Tanzania APHTA kwa kushirikiana na hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mwanza Sekou Toure, kilitoa fursa kwa wananchi kupima afya zao bure kwa magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo kisukari.
Maadhimisho hayo kwa mkoa wa Mwanza yalifanyika kwenye uwanja wa Nyamagana ambapo mgeni rasmi ambaye ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt.Leonard Subi anawahimiza wananchi kuzingatia ulaji sahihi wa vyakula pamoja na kufanya mazoezi ili kujiepusha na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwemo kisukari.
Hata hivyo wananchi wanahimizwa kupima afya zao mara kwa mara ili kuepuka madhara wanayoweza kukumbana nayo kutokana na magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo kisukari, ikizingatiwa kwamba watanzania tisa kati ya 100 wenye umri wa miaka 25 na kuendelea wana ugonjwa wa kisukari ambapo kati ya hao tisa, ni wagonjwa wawili tu wenye kutambua kwamba wanaugua ugonjwa huo.
Wednesday, November 15, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. ...
-
Kaimu Naibu Mraijis wa Vyama vya Ushirika nchini, Charles Malunde Warajis Wasaidizi wa Vyama vya Ushirika wa Mikoa wametakiwa kuwash...
-
HOTUBA YA KUTANGAZA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE KATIKA JIMBO LA ISIMANI KWA TIKETI YA CHAMA CHA MAPINDUZI MWAKA 2015 UTANGULIZI UTA...
-
Moja ya kibanda cha biashara kilichofungiwa na kuwashwa umeme na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, katika kij...
-
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mh. Kisare Matiku Makori Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mh. Kisare Matiku Makori akitoa tone la chanjo kuashiria...
Powered by Blogger.
0 comments:
Post a Comment