METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, September 13, 2017

Serikali Kuendelea Kuboresha Mazingira ya Wafanyabiashara Nchini

19
Na: Lilian Lundo – MAELEZO – Dodoma

Serikali kuendelea kuboresha mazingira ya kufanyia biashara ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kuvutia wafanyabiasha wa ndani na nje ya nchi.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ameyasema hayo leo mjini Dodoma wakati akizindua  awamu ya tano ya programu ya maboresho ya usimamizi wa fedha za Umma 2017/18  na 2021/22.

 Akifafanua Mhe. Samia amesema kwamba katika kuhakikisha kunakuwepo na usimamizi  mzuri wa fedha za umma, Serikali ya Awamu ya Tano itahakikisha  kuwa wafanyabishara wote wanatumia mfumo wa kielekroniki kulipa kodi.

Aidha amesema kuwa Serikali itaendelea kupunguza matumizi ya fedha katika Wizara, Taasisi na Idara zake ili fedha hizo ziweze kutumika katika kuboresha huduma za jamii.

Naye, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amesema kuwa programu ya maboresho ya usimamizi wa fedha umeleta mafanikio makubwa ambapo umeongeza makusanyo na mapato ya Serikali Tanzania Bara na Visiwani.

“Awamu hii ya Tano ya program ya maboresho ya usimamizi wa fedha za Umma itaweka nguvu na kuimarisha ofisi za wakaguzi wa mahesabu na kutambua mapungufu yaliyopo  katika ofisi hizo,” alifafanua Dkt. Mpango.

Vile vile katika awamu hii  maboresho ya kazi za wakaguzi wa ndani katika  Wizara, Taasisi, Idara pamoja mamlaka ya Serikali za mitaa nchini.

Maboresho ya programu ya usimamizu wa fedha za Umma ulianza mwaka 1998 ikiwa ni awamu ya kwanza ambayo ilihusisha uthibiti matumizi ya Serikali na kuchangia kukuza uchumi endelevu.

Awamu ya pili ilifanyika mwaka 2004 – 2008 ambayo ilijikita katika kuboresha usimamizi wa fedha za umma kwa kutumia viwango vya kimataifa. Awamu ya tatu ilifanyika mwaka 2008 – 2012 ambayo ilihusisha katika kuhakikisha mbinu na mifumo iliyowekwa awamu ya kwanza inaoanishwa na kutumika ipasavyo kuleta matokeo yaliyokusudiwa na awamu ya nne ilikuwa mwaka 2012-2017 ambayo ilenga katika nidhamu katika usimamizi wa fedha za umma na kutoa huduma bora kwa Umma ili kuleta maendeleo endelevu
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com