Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa Mhe George B. Simbachawene (Mb) akizungumza na wananchi katika shule ya sekondari Ipera, kata ya Ipera,
kijiji cha Kinusi, wilayani Mpwapwa wakati wa ziara yake mwishoni mwa juma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe George B. Simbachawene (Mb) akiangalia mmea aina ya fungi ambaye ni kingdom animalia katika shule ya sekondari Ipera, kata ya Ipera, kijiji cha Kinusi, wilayani Mpwapwa wakati wa ziara yake mwishoni mwa juma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe George B. Simbachawene (Mb) akikagua jengo la bweni katika shule ya sekondari Kibakwe wilayani Mpwapwa wakati wa ziara yake mwishoni mwa juma
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa Mhe George B. Simbachawene (Mb) akiangalia mmea aina ya fungi
ambaye ni kingdom animalia katika shule ya sekondari Ipera, kata ya Ipera,
kijiji cha Kinusi, wilayani Mpwapwa wakati wa ziara yake mwishoni mwa juma.
Na Fred J. Kibano
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe George B.
Simbachawene (Mb) ameziagiza Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini kutumia fedha
za Maendeleo za Mamlaka ya Serikali za Mitaa (LGDG) zilizotengwa katika mwaka
wa fedha 2017/2018 kiasi cha shilingi bilioni 249 kwa nchi nzima zitumike kwa
ajili ya maendeleo ikiwa ni pamoja na asilimia 10 iliyotengwa kwa ajili ya
kuwajengea uwezo watumishi wa Mamlaka hizo.
Akiongea
katika ziara yake aliyoifanya mwishoni mwa juma, Mhe. Simbachawene amesema kwa
sasa hatuna budi kuangalia maendeleo ya Taifa kwanza na sio kuendelea kulipia
mambo yasio ya lazima ikiwa ni pamoja na kutenga fedha za kujengewa uwezo hali
ambayo si sahihi kwa maslai ya Taifa na Serikali ya awamu ya tano.
“Halmashauri
zote nchini, zitumie hii fedha ya LGDG (Fedha za Maendeleo za Mamlaka za
Serikali za Mitaa), fedha ile ya maendeleo kwa ajili ya maendeleo na si
vinginevyo, na maendeleo ninayoagiza kwa Halmashauri zote nchini yawe yanalenga
kumaliza maboma yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi kama miradi iliyopita”
Ameyataja
mfano wa baadhi ya maboma ambayo yanastahili kutumia fedha hizo yaliyopo
wilayani Mpwapwa ni kama madarasa ya shule ya msingi Wangama, Maabara ya Mbuga
sekondari, shule ya msingi Shikizi na mengineyo ambayo yamejengwa kwa nguvu za
wananchi.
Mchanganuo
wa fedha hizo ambao ni shilingi bilioni 249 asilimia 80 ni kwa ajili ya
shughuli za maendeleo, asilimia 10 kwa ajili ya kazi za usimamiaji na asilimia
10 kwa ajili ya kujengewa uwezo ambazo zimekatwa na kuwekwa kwa ajili ya
maendeleo.
“Lakini
asilimia 10 ambayo inasema ni kujengewa uwezo, ambayo ni watu wanakwenda
semina, warsha, mara waite ‘workshop’, hii hapana, hii fedha yote iende kwa
ajili ya miradi ya wananchi hasa kwenye maboma.
Tunayo
maboma mengi sana, hasa sekta ya afya, elimu na mengineyo”
Mhe.
Waziri Simbachawene amesisitiza kuwa hata wakati akihitimisha hotuba yake
katika bunge la bajeti alitoa kauli ya matumizi ya fedha hizo. “ Nilipokuwa
nafunga hotuba yangu kwenye bunge la bajeti nilielekeza asilimia 60 tuipeleke
kwenye miradi ya afya na kwa hivyo narudia hapa kusema asilimia inayobaki yote
iedne kwenye miradi ya elimu, kasoro ile asilimia 10 usimamiaji kwa sababu ni
lazima miradi ili iwe mizuri, lazima isimamiwe” , alisema.
Aidha,
amesema Serikali itatoa waraka maalum kuonyesha mchanganuo wa matumizi ya fedha
hizo maalum za maendeleo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ndani ya mwaka huu
wa fedha wa Serikali.
Mheshimiwa
Simbachawene anafanya ziara katika Mamlaka za Serikali za Mitaa hasa maeneo ya
vijijini ili kujionea hali halisi ya utendaji, migogoro ya ardhi, utunzaji wa
mazingira, huduma kwa wananchi na ukamilishaji wa miradi ya maendeleo ambapo
mwishoni mwa wiki ametembelea kata za Mbuga, Kibakwe na Ipera zenye vijiji
kadhaa wilayani Mpwapwa kama sehemu ya kazi zake za kujionea maendeleo ya
wananchi na kero zao.
0 comments:
Post a Comment