Naibu waziri Ofisi ya Waziri
Mkuu- Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe ANTHONY
MAVUNDE kitembelea karakana wakati alipozindua Mafunzo ya UTAMBUZI WA
UJUZI ULIOPATIKANA NJE YA MFUMO RASMI kwa Vijana 847 kutoka Mikoa ya
Mtwara, Lindi, Morogoro, Pwani, na Dar es Salaam mkoani Mtwara.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri
Mkuu- Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe ANTHONY
MAVUNDE akizindua Mafunzo ya UTAMBUZI WA UJUZI ULIOPATIKANA NJE YA MFUMO
RASMI kwa Vijana 847 kutoka Mikoa ya Mtwara, Lindi, Morogoro, Pwani, na
Dar es Salaa.
……………………………………………………………………………
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri
Mkuu- Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe ANTHONY
MAVUNDE amezindua Mafunzo ya UTAMBUZI WA UJUZI ULIOPATIKANA NJE YA MFUMO
RASMI kwa Vijana 847 kutoka Mikoa ya Mtwara, Lindi, Morogoro, Pwani, na
Dar es Salaam mafunzo yaliyozinduliwa Mkoani Mtwara.
Mhe Mavunde amewataka Vijana kuchangamkia fursa wasisubiri serikali itoe matangazo, iwatafute, iwakusanye, iwape ujuzi Msingi wa maisha ya kijana unaanzia hapa Kijana wa kitanzania jiamini, timiza wajibu wako
OMBI KWA VIJANA Vijana waliopata fursa ya
kuingia kwenye Mafunzo Haya, kutumia vizuri fursa hii kwa kuwa WAAMINIFU
na KUWAJIBIKA kama msingi wa mafanikio, Waache Tamaa waende kwa Hatua.
“ni kaburi peke yake watu waanza kuchimba kuanzia juu kwenda
Chini, lakini maisha yananzia Chini kwenda juu” amesisitiza Mhe Mavunde.
Mafunzo haya yanatolewa na Serikali kupitia Fedha za walipata
KODI, hivyo wahakikishe wanatumia vizuri fedha zinazotolewa katika
mafunzo Haya mana ni fedha za watanzania, Serikali ya Mhe John Pombe
Magufuli imedhamiria kuwekeza kwa vijana kwa kuwajengea UWEZO vijana ili
waweze kunufaika na maendeleo ya rasilimali zilizopo nchini.
Imetolewa na kitengo cha mawasiliano Serikalini
Ofisi ya Waziri Mkuu kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu.
24/08/2017
24/08/2017
0 comments:
Post a Comment