Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua ujenzi wa daraja ya Nyatanga lililopo katika kijiji cha Nyani wilayani Kisarawe
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akipata maelezo ya ujenzi wa barabara ya Mzenga-Gwata
Ujenzi unaoendelea wa daraja la Kologombe
wilayani Kisarawe
WANANCHI wa vijiji vya Dololo na Gwata katika kata ya Mafizi
wilayani Kisarawe wameishukuru serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dk.
John Magufuli wa kuwaboresha barabara inayotoka Mzenga hadi Dololo kupitia
Gwata.
Wakazi hao walitoa shukurani hizo wakati wa ziara ya Naibu
Waziri wa Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo ya kukagua miradi ya maendeleo iliyofanywa
na Naibu Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo hilo.
Wamemshukuru Mbunge wao kwa kuwapigania ambapo kwasasa barabara
hiyo inaboreshwa kwa kuweka vizuri katika maeneo korofi na kukamilisha
ujenzi wa madaraja mawili la kipora, Nyatanga, na kwasasa serikali inakamilisha
ujenzi wa daraja la Kologombe.
Akizungumza na wananchi hao, Naibu Waziri Jafo amewapongeza
viongozi na watendaji kwa kusimamia vyema miradi mbalimbali inayotekelezwa
wilayani humo.
Aidha amewapongeza wakandarasi wanaojenga daraja la
Kologombe kwa kazi nzuri ya ujenzi wa daraja hilo.
0 comments:
Post a Comment