TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imesikitishwa na kitendo
kilichofanywa na Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli Tanzania (Rahco)
kubomoa nyumba zaidi ya 200 zilizojengwa pembezoni mwa reli eneo la
Buguruni, Machi 11, mwaka huu.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Tume hiyo, Bahame Nyanduga, kampuni hiyo
ilitekeleza ubomoaji huo, wakati ikiwa na taarifa ya mwito wa Tume
kuhusu malalamiko ya wananchi wa eneo hilo.
Malalamiko hayo yanahusu uhalali wa makazi yao kuwa nje ya mita 15 au
mita 30 kama Sheria ya Reli Namba 4 ya Mwaka 2002, inavyoelekeza.
“Ubomoaji wa nyumba hizi ulianza tangu Machi 11 saa nne asubuhi
katika Mtaa wa Madenge, Kata ya Buguruni na uliendelea Machi 12, mwaka
huu katika mitaa ya Faru, Mtakuja na Mtambani katika kata ya Mnyamani,”
alisema Nyanduga.
Alisema Februari 22, mwaka huu, Kamati iliyoundwa na wananchi wa
Mnyamani ilifika katika Ofisi za Tume na kusajili lalamiko lao kwamba
nyumba zao ziliwekwa X kuashiria kuvunjwa bila wao kujulishwa.
Alisema baada ya malalamiko hayo, Tume iliwasiliana na uongozi wa
Serikali ya Mtaa wa Mtambani, Faru na diwani wa Mnyamani, uliosema
haukuwa na taarifa kutoka Rahco kama watabomoa nyumba hizo.
“Tume iliwasiliana na Uongozi wa Rahco ulisema hilo ni eneo la mradi
wa Reli ya Standard Gauge na kwamba hata ramani ya Mnyamani inaonesha
eneo hilo lipo ndani ya mita 30 za reli tofauti na madai ya wananchi,”
alisema.
Mwenyekiti huyo alisema Tume iliziandikia pande zote mbili barua
Machi 7, mwaka huu kuzitaka ziwasilishe vielelezo vyao ifikapo Machi 13,
mwaka huu na kuzitaka pande zote mbili kuwasili mbele ya Tume ili
zisikilizwe ifikapo Machi 14, mwaka huu.
Alisema baada ya Rahco kupata barua ya Tume ilijibu kuwa haiwezi
kuwasilisha vielelezo kwani mwanasheria wao alikuwa safarini ingawa
Rahco ilisema utaratibu wa kubomoa nyumba hizo ulifanyika kwa
kushirikisha wawakilishi mbalimbali.
Tuesday, March 14, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. ...
-
Mkuu wa Wilaya ya Songwe Samuel Jeremia Opulukwa akinawa mikono kabla ya kuingia katika Zahanati ya Saza itakayotumika kutibu endapo ata...
-
MKURUGENZI wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Tanzania (DCI), Robert Boaz Mikomangwa amesema Jeshi la Polisi nchini Tanzania na vyombo vingi...
-
Naibu waziri Kilimo Mhe. Omari T. Mgumba (Mb) akiwa ofisi ya mkuu wa mkoa wa arusha alipokutana na wataalamu wa kilimo ,ushirika na ...
Powered by Blogger.
0 comments:
Post a Comment