UJENZI wa laini mpya ya umeme wenye nguvu ya Kilovolti 33 kutoka
Chalinze kwenda Mlandizi eneo lenye urefu wa kilomita 45 umekamilika
mwishoni mwa wiki.
Kukamilishwa kwa ujenzi huo kutawezesha pampu mpya za mtambo wa maji
wa Ruvu Juu kusukuma jumla ya lita milioni 196 za maji safi kwa siku.
Taarifa iliyotolewa ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es
Salaam (Dawasa) ilisema, Mamlaka hiyo kupitia mkandarasi wake wa WABAG
kutoka nchini India akishirikiana na mkandarasi msaidizi, kampuni ya M/S
Mollel Electrical ya nchini, ilikuwa na kazi ya kupitisha nyaya za
umeme ili ziingie katika eneo la mtambo.
Imesema ili kazi hiyo ifanyike pasipo kuleta madhara, laini maalumu
kwa ajili ya umeme mkubwa wa kilovolti 33 inayoendesha mitambo ya maji
ya Ruvu Chini na Ruvu Juu ililazimika kuzimwa kwa kuwa laini hiyo mpya
inapita chini na juu ya laini hizo.
Imebainisha kuwa, kitaalamu ni hatari kufanya kazi ya kupitisha nyaya
za umeme chini au juu ya laini za umeme nyingine kubwa zikiwa na umeme.
Mtambo sasa utahitaji jumla ya 16MVA za umeme ili kusukuma maji safi
yanayozalishwa kwa asilimia 100 na kazi iliyobaki hivi sasa ni kuunga
laini hiyo mpya katika sub-station ya Chalinze ili pampu zote ziweze
kufanya kazi.
Taarifa hiyo ilibainisha kuwa Dawasa inalishukuru Shirika la Umeme
Tanzania (Tanesco) kwa ushirikiano na ushauri wa kitaalamu kuhusu
masuala ya umeme ambao imekua ikiutoa ili kukamilisha kazi hiyo.
Aidha, imeweka wazi kuwa, vifaa vyote muhimu kwa ajili ya kukamilisha
kazi hiyo viliandaliwa na kuwa kazi hiyo imekamilika na umeme
umewashwa.
Tuesday, March 14, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. ...
-
Mkuu wa Wilaya ya Songwe Samuel Jeremia Opulukwa akinawa mikono kabla ya kuingia katika Zahanati ya Saza itakayotumika kutibu endapo ata...
-
MKURUGENZI wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Tanzania (DCI), Robert Boaz Mikomangwa amesema Jeshi la Polisi nchini Tanzania na vyombo vingi...
-
Naibu waziri Kilimo Mhe. Omari T. Mgumba (Mb) akiwa ofisi ya mkuu wa mkoa wa arusha alipokutana na wataalamu wa kilimo ,ushirika na ...
Powered by Blogger.
0 comments:
Post a Comment