METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, February 15, 2024

SERIKALI INAENDELEA NA UPEMBUZI YAKINIFU NA USANIFU BONDE LA BUYUNGU.



Na Saida Issa, Dodoma

SERIKALI kupitiaTume ya Taifa ya Umwagiliaji inaendelea na kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika bonde la Buyungu linalojumuisha Skimu za Katengera, Muhwazi, Ruhwiti, Ruhuru, Mgunzu, Kayonza, Lukoyoyo, Chulanzo, Asante Nyerere na Kilimo Kwanza.

Hayo yameelezwa Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri kilimo David Silinde alipokuwa akijibu swali lililoulizwa na Mbunge wa Buyungu Aloyce kamamba alipouliza 
Je,ni lini Skimu za Umwagiliaji za Katengera, Muhwazi, Gwanumbu na Ruhwiti katika Wilaya ya Kakonko zitakarabatiwa. 

Kazi za upembuzi yakinifu na usanifu zinatarajiwa kukamilika mwezi Mei, 2024.

"Kukamilika kwa kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika skimu hizi kutawezesha kupatikana kwa gharama halisi za ujenzi na ukarabati, hivyo kuwekwa kwenye mpango wa ujenzi na bajeti,

Mheshimiwa Spika, Mradi wa umwagiliaji Gwanumbu umeendelezwa kwa kujengewa mfereji mkuu, mradi huu unahitaji kufanyiwa usanifu wa miundombinu ambayo haijakamilika,"amesema.

Aidha amesema kuwa Katika mwaka wa fedha 2024/2025 Mradi wa umwagiliaji Gwanumbu utaingizwa kwenye mpango wa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili kujua gharama halisi za ukarabati kabla ya kuingizwa kwenye mpango wa ujenzi na bajeti.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com