Na Mathias Canal – Ikungi, Singida
VIONGOZI wa Dini Mkoani
Singida wametakiwa kuwa mstari wa mbele kukemea vitendo vya mmomonyoko wa
Maadili ambavyo ni kinyume na mila na desturi na kwamba watumie nafasi yao kuibadilisha mitazamo juu ya utamaduni huo.
Kauli hiyo imetolewa April
16, 2023 na Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Mhe. Miraji Mtaturu wakati
akizungumza na viongozi wa dini ya Kiislamu katika msikiti wa mji wa Makyungu
Wilayani Ikungi ambapo amesema Viongozi wa Dini wana nafasi kubwa ya kuiusia
jamii kufuata Maadili yanaelezwa kwenye vitabu vitukufu.
Mhe. Mtaturu
alisisitiza kuwa baadhi ya watu wamekuwa wakitumia kivuli cha haki na usawa
jambo linalosababisha kukithiri kwa vitendo vinavyokiuka maadili ya Tanzania
ikiwemo Mapenzi ya Jinsia moja.
“Viongozi wa Dini
Mnanguvu ya ushawishi kwa waumini (Wananchi), kuna hili suala ya Haki na usawa
ambalo baadhi ya watu wamekuwa wakitumia kivuli hicho kukiuka maadili yetu,
niwaombe Viongozi wangu wa Dini mlikemee na kulipinga vikali hili”Alisema Mhe.
Mtaturu.
Katika Hatua nyingine
Mhe. Mtaturu aliongeza kwa kuwataka viongozi wa Msikiti huo kubuni Miradi ya
maendeleo badala ya kutegemea wafadhili jambo ambalo linarudisha nyuma
maendeleo ya Waislaamu wa eneo hilo.
Aliongeza kuwa hivi
karibuni ataletwa mtaalamu wa michoro kwaajili ya kulipangilia eneo la Msikiti
Makyungu ili kuongezea thamani kwa kujenga Vibanda vya kukodisha wafanyabishara
pamoja na Ukumbi wa Mikutano utakaowaingizia kipato waumini hao.
Kuhusu Miradi Mhe.
Mtaturu alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za kutekeleza
miradi hiyo ikiwemo Sekta ya nishati, Miundombinu ya Barabara na Mawasiliano,
Maji, Shule na Afya kwenye wilaya hiyo na kuwahakikishia kuendelea kuwasemea
wananchi wa Jimbo la Singida Mashariki kwa ujumla.
0 comments:
Post a Comment