METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, March 28, 2023

TANESCO YAPONGEZWA KWA KUZALISHA, KUSAFIRISHA NA KUSAMBAZA UMEME NCHINI

Watendaji mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati, Shirika la umeme Tanzania pamoja na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania, wakiwa kwenye mafunzo ya kuwajengea uelewa sawa wa wajumbe wapya wa kamati ya Nishati na Madini na kuwaongezea uelewa wale waliokuwepo katika kamati hiyo, katika sekta ya Umeme, Mafuta na Gesi.



Watendaji mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati, Shirika la umeme Tanzania pamoja na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania, wakiwa kwenye mafunzo ya kuwajengea uelewa sawa wa wajumbe wapya wa kamati ya Nishati na Madini na kuwaongezea uelewa wale waliokuwepo katika kamati hiyo, katika sekta ya Umeme, Mafuta na Gesi.


Mkurugenzi wa Shirika la Petroli Tanzania, Mussa Makame, akiwasilisha mada kwenye mafunzo ya kuwajengea uelewa sawa wa wajumbe wapya wa kamati hiyo na kuwaongezea uelewa wale waliokuwepo katika sekta ya Mafuta na Gesi nchini.


Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania, Maharage Chande, akiwasilisha mada kwenye mafunzo ya kuwajengea uelewa sawa wajumbe wapya wa kamati hiyo na kuwaongezea uelewa wale waliokuwepo katika sekta ya Umeme nchini.


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Athumani Selemani Mbuttuka akiwa kwenye mafunzo ya kuwajengea uelewa sawa  wajumbe wapya wa kamati hiyo na kuwaongezea uelewa wale waliokuwepo katika sekta ya Umeme, Mafuta na Gesi.


Naibu Waziri wa Nishati, Wakili Stephen Byabato akiwa kwenye mafunzo ya kuwajengea uelewa sawa wajumbe wapya wa kamati hiyo na kuwaongezea uelewa wale waliokuwepo katika sekta ya Umeme, Mafuta na Gesi.


 

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Dunstan Kitandula akizungumza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uelewa sawa kwa wajumbe wapya na kuwaongezea uelewa wale waliokuwepo katika sekta ya Umeme, Mafuta na Gesi.



Na Godfrey Mwemezi, Dodoma

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imepongeza uongozi wa Shirika la Umeme nchini (TANESCO) kwa jitihada zake za uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme nchini.

Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Dunstan Kitandula ametoa pongezi hizo Jijini Dodoma wakati Kamati hiyo ilipokuwa katika semina ya kujengewa uwezo katika masuala ya umeme, mafuta na gesi, Machi 25 hadi 26, 2023.

‘’Sisi Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini tunaipongeza Wizara ya Nishati na Shirika la umeme Tanzania kwa juhudi wanazofanya katika uzalishaji, usafirishaji na usambazaji umeme nchini, jambo ambalo linaongeza ukuaji wa uchumi wa Taifa letu kwa kasi,” amesema Kitandula.

Akizungumza na wajumbe wa Kamati hiyo, Naibu Waziri wa Nishati, Wakili Stephen Byabato amesema kuwa lengo la semina hiyo ilikuwa ni kutoa uelewa sawa kwa wajumbe wapya na kuwaongezea uelewa wale waliokuwepo katika kamati hiyo.

Amesema semina hiyo imeandaliwa na Wizara ya Nishati kupitia TANESCO pamoja na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) ili kuendelea kuwaimarisha wajumbe wa kamati hiyo kwa kuwa ndio wanaoishauri serikali katika sekta ya umeme, mafuta na gesi.

Wakati akifunga semina hiyo, Kitandula ameipongeza Wizara na taasisi hizo mbili kwa kuandaa mafunzo hayo yaliyokuwa na lengo la kuwajengea uelewa wajumbe wa kamati hiyo ya Bunge.

Baadhi ya waliohudhuria semina hiyo ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Athumani Selemani Mbuttuka, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Maharage Chande, Mkurugenzi wa TPDC, Mussa Makame pamoja na watendaji wengine wa Wizara na taasisi hizo.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com