Kikao hicho kimefanyika leo tarehe 11 Machi 2023 Bungeni jijini Dodoma na kuhudhuriwa na viongozi, Menejimenti ya Ofisi ya Rais TAMISEMI wakiongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe, Angellah Kairuki.
Pamoja hayo, Kamati imepokea taarifa ya Utekelezaji wa Miradi tisa ya maendeleo itakayotembelewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI kuanzia tarehe 14 -19 Machi 2023.
Kamati za Kudumu za Bunge zinaendelea na vikao ambavyo vimeanza tarehe 10 Machi 2023 na vinatarajiwa kumalizika tarehe 31 Machi 2023 kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Bunge.
0 comments:
Post a Comment