Timu ya Wataalam wa Maji kutoka Bonde la Maji kanda ya kati kituo cha Singida wakiongozwa na Ndugu Mushuro wameendelea na kazi ya utafiti kwenye kijiji Cha Damankia ili kujua ubora na wingi wa maji maeneo hayo hatimae mitambo ya kuchimba visima virefu iweze kufika kwa ajili ya kuwapatia wananchi maji safi na salama kwenye jimbo la Singida Mashariki.
Kazi itafanyika kwa wiki hii nzima kuanzia tarehe 3 Januari 2022 kwenye vijiji vya Msule, Mampando, Ujaire, Mang'onyi na Mbwanjiki.
Mbunge wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu akiongea na mwandishi wetu amemshukuru sana mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutimiza dhamira yake ya kuwapatia wananchi maji safi na salama.
#SingidaMashariki#MaendeleoKipaumbeleChetu#
0 comments:
Post a Comment