Waziri wa Kilimo Mhe Prof. Adolf Mkenda (Mb) akisisitiza jambo wakati wa kikao cha kazi na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wzara ya Kilimo, pamoja
na Wakuu wa Bodi na Taasisi kilichofanyika katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo
Jijini Dodoma, leo tarehe 9 Septemba 2021. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Waziri wa Kilimo Mhe Prof. Adolf Mkenda (Mb) amempongeza Katibu
Mkuu wa wizara ya Kilimo Ndg Andrew Massawe kwa kuzisimamia kwa weledi mkubwa Bodi
na Taasisi zilizo chini yake hivyo kuendeleza uwajibikaji kuhakikisha kuwa
sekta ya kilimo inaendelea kuimarika.
Amesema kuwa wananchi wana imani kubwa na Wizara ya kilimo hivyo
kuna kila sababu ya kuongeza weledi katika uwajibikaji ikiwa ni pamoja na kuwasajili
wakulima ili kuwatambua jambo litakaloiwezesha serikali kuwatambua wakulima hao
na kuweza kuwahudumia.
Waziri wa Kilimo Mhe Prof. Adolf Mkenda (Mb) ametoa maelekezo hayo
wakati wa kikao cha kazi na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wzara ya Kilimo, pamoja
na Wakuu wa Bodi na Taasisi kilichofanyika katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo
Jijini Dodoma.
Akizungumza
kuhusu Tija na uzalishaji wa mazao nchini Waziri Mkenda amesema kuwa Kiwango
cha uzalishaji na tija kwenye mazao mengi hapa nchini bado kipo chini. Kwa
mfano, uzalishaji wa korosho kwa sasa ni wastani wa kilo 5 hadi 10 kwa mti
ikilinganishwa na tija ya juu ya kilo 35 kwa mti inayoweza kufikiwa kulingana
na viwango vya kitaalam.
Baadhi ya sababu zinazosababisha kuwepo kwa tija ndogo kwenye
mazao ni pamoja na Matumizi madogo na yasiyokuwa sahihi ya pembejeo, Uwekezaji
mdogo kwenye tafiti za kimaendeleo,Huduma duni za ugani, naKuyumba kwa masoko
ya mazao kwenye baadhi ya misimu.
Amesema kuwa Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na wadau
imeendelea na jitihada za kuongeza uzalishaji na tija katika mazao ya kimkakati
ikiwemo korosho ili kuongeza kipato cha mkulima na taifa kwa ujumla.
“Mfano kwenye zao la Pamba kwa sasa wanaendelea na kampeni
kubwa ya kuongeza tija na uzalishaji kwa kumtumia Balozi wa Pamba Ndg Aggrey
Mwanri ambapo wameanza kampeni hiyo mkoa wa Simiyu, Shinyanga na kwa sasa
wataelekea Geita kabla ya kuelekea katika mikoa mingine” Amesisitiza Waziri
Mkenda
Katika kikao kazi hicho Waziri Mkenda amempongeza
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Hussein Bashe kwa usimamizi na uwajibikaji uliotatua
muarobaini wa kadhia ya kuchelewa kwa viuatilifu na hatimaye kufanya juhudi
kubwa k.uhakikisha viuatilifu vinafika kwa wakati kwa wakulima wa zao la
korosho.
Kwa upande
wake Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Hussein Bashe (Mb) ameitaka Bodi ya Nafaka na
Mazao Mchanganyiko-CPB na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula-NFRA kuhakikisha
kuwa inawafuata wateja wakati wa ununuzi wa nafaka ili kuwarahisishia huduma katika
maeneo walipo.
Kuhusu zao
la alizeti Mhe Bashe amesema kuwa serikali inaendelea na juhudi kubwa
kuhakikisha kuwa mbegu za alizeti zinapatikana kwa wingi na kwa wakati.
MWISHO
Congratulations hon minister for the job well done. Agriculture is the engine sector
ReplyDelete