METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, August 31, 2020

ARUSHA FESTIVAL YAWEKA REKODI JIJI LA ARUSHA,MAELFU YA WANANCHI WAMIMINIKA KUSHUHUDIA



Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe Kenani Kihongosi akizungumza na Maelfu ya wakazi wa Wilaya ya Arusha na nje ya Wilaya hiyo, waliojitokeza katika Tamasha la “Arusha Festival” lililoandaliwa na ofisi yake

Maelfu ya wakazi wa Wilaya ya Arusha na nje ya Wilaya hiyo, waliojitokeza katika Tamasha la “Arusha Festival” lililoandaliwa na ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Kenani Kihongosi wakifuatilia tamasha hilo.

Na Innocent Natai

Akifungua tamasha hilo lililokuwa na lengo la kuonyesha fursa za burudani na uchumi kwa wasanii na wananchi wa Arusha,Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mh Kenani Kihongosi ambae ndie aliyefungua na kufunga tamasha hilo amewahakikishia wakazi wa Arusha Kuwapa ushirikiano zaidi na kuibua vipaji vipya na kuviendelea kwani sanaa ni Ajira

 

Aidha Dc Kenani amewataka wakazi wa Arusha na Tanzania kwa ujumla kuzidi kuiunga mkono serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli iliyofanya na inayozidi kufanya mambo makubwa katika sekta ya sanaa na burudani kwa ujumla  ambayo pia imelenga kuendeleza sanaa hapa nchini na kuwafanya wasanii kufaidika na sanaa zao.

 

Dc Kenani amesema ni dhamira ya ofisi yake kuhakikisha Wilaya ya Arusha inakuwa Wilaya ya mfano kwa kuwa na maendeleo,usalama na amani huku pia wananchi wake wanaofanya sanaa mbalimbali wakizidi kuendeleza vipaji vyao kupitia matamasha mbalimbali  kama lililoandaliwa na Ofisi yake ili wanufaike na Sanaa zao

 

Aidha Wananchi wa Arusha wamepongeza Ubunifu huo na wameipongeza serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe rais Dkt JOHN POMBE MAGUFULI kwa kuwajali Vijana na kuweka historia Isiyofutika Katika Wilaya ya Arusha kwa uwepo wa Tamasha Hilo.

 

Tamasha La Arusha festival lililoandaliwa na Ofisi Ya Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe Kenani Kihongosi  lililohudhuriwa na Maelfu ya wakazi wa Viunga vya Jiji la Arusha na hata nje ya Jiji hilo limefanyika katika viwanja vya Soko la Kilombero huku lilitumbuizwa na wasanii Maarufukutoka Mkoa wa Arusha na nje  wakiwemo Dipper Rato,Dogo Janja,Marioo,Beka Flavour,Kala Jeremiah,Baraka The Prince,Meda Classic na wengine lukuki.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com