METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, May 13, 2020

BAKWATA YAMPONGEZA MBUNGE ILEMELA



Baraza kuu la waislamu Tanzania (BAKWATA) wilaya ya Ilemela limempongeza mbunge wa jimbo hilo Mhe Dkt Angeline Mabula kwa kujali na kuthamini, wajane, yatima, wazee, walimu wa dini ya kiislamu, mashekh, masikini na watu wasiojiweza katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Kauli hiyo imetolewa na shekh wa wilaya ya Ilemela Husein Mwamba  katika viwanja vya shule ya msingi Kitangiri wakati wa zoezi la ugawaji sadaka ya futari kwa wagane, wajane, yatima, wazee, walemavu na watu wasiokuwa na uwezo kutoka kata 19 za wilaya ya Ilemela ambapo shekh huyo amempongeza mbunge Dkt Mabula kwa kujitoa kusaidia watu wasiokuwa na uwezo huku akiwataka viongozi wengine na wadau kuona haja ya kusaidia makundi maalum katika jamii yenye uhitaji. 

‘.. Waislamu wapo katika ibada ya kutekeleza amri ya mola wao, Kwa mapenzi makubwa akaona walau apate wazee, mayatima, wajane na wale wasiojiweza ili atoe sadaka kuwawezesha watekeleza ibada yao kwa salama na amani, Mbunge hakuangalia kabila, dini wala rangi wapo  wenye uwezo wa kupata futari na wapo wasioweza, Tuna wajibu wa kumuombea dua na kumpongeza ..’ Alisema

Aidha shekh huyo akawataka waislamu hao kushukuru kwa futari iliyotolewa na kuendelea kumuombea dua mbunge huyo kwa moyo wake wa kujali na kushirikiana na jamii katika mambo mbalimbali huku akikiri kupokea barakoa na ndoo 42 zitakazogawanywa katika misikiti yote iliyopo ndani ya wilaya hiyo kama sehemu ya kujikinga na ugonjwa wa virusi vya Corona zilizotolewa na mbunge huyo.

Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula amewashukuru wadau alioshirikiana nao katika kufanikisha utoaji wa sadaka hiyo akiwemo mkurugenzi wa GBP Ndugu Rashid Seif Sudi, Mr Brown Mteta Peter wa Nakiete Pharmacy ya Dar es Salaam, Olympic Petroleum, Charles Mlowa wa Tropical Company, Samuel Melishek Mollel wa Nakoroi Ltd Dar es Salaam, KCB Bank Tanzania Ltd, Princes Pharmaceutical Ltd na Tarmal Industries Ltd huku akitoa fursa kwa wadau wengine watakaohitaji kushirikiana nae katika kusaidia utatuzi wa kero na changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii. 

Akihitimisha katibu wa BAKWATA wilaya ya  Ilemela Shekh Sadick Mchora mbali na kumpongeza mbunge huyo akaongeza kuwa ipo haja kwa waislamu na viongozi wa dini kuendelea kukumbushana juu ya kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa Covid-19 ili kuzuia maambukizi mapya ya ugonjwa huo.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com