METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, March 26, 2020

SHAKA: Heko JPM kwa kuipigania Zimbabwe

Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Morogoro  kimefurahishwa na msimamo idara  uliotolewa na Waziir Mkuu Kassim Majaliwa  kwa niaba ya serikali ya Rais Dkt John Magufuli , unaozitaka  Nchi  wanachama  za SADC kusimama pamojao na Zimbabwe mpaka  pale  vikwazo dhalimu  vya kiuchumi nchini humo zitakapoondolwa.

Kimesema wakati huu dunia nzima ikikumbwa na janga la kusambaa kwa virusi vya Corona huku huduma za kibinadamu zikihitajika kwa kiasi kikubwa haipendezi kuishuhudia  zimbabwe ikiendelea kuwekewa vikwazo vya kiuchumi. 

Matamshi hayo yametamkwa  jana na Katibu wa CCM  Mkoa Morogoro  Shaka Hamdu Shaka ofisini kwake  akiipongeza  hotuba  ya Waziri Mkuu Majaliwa aliyotoa wakati alipofungua kikao cha mawaziri wa Afya wa Jumuiya ya Maendeleo ya   kiuchumi Kusini mwa Afrika (sadc).

Shaka alisema vikwazo hivyo  vinaapaswa  kuondosha kwa hiari kwa  kujali haki na kuthamini ubinadanu lakini  kipindi  hiki wakati dunia ikikabiliwa na mazingira ya kijografia yenye joto kali na mtafaruku, vifo  na majanga, vikwazo hivyo ni manyanyaso na dhulma kwa binadamu wasio na hatua.

Amefahamisha kuwa kama serikali ya CCM ilivyoshiriki harakati za kupigania haki na usawa mahali popote dunia ambako  haki ,usawa na uhuru wa watu ulifungwa vitanzi, vikwazo vya kiuchumi dhidi  zimbabwe pia  havipaswi kuwepo.

'Hotuba ya Waziri Mkuu Majaliwa Kwa niaba ya Mhe Rais Magufuli ilikuwa ya kijasiri na kizalendo . CCM mkoa wa Morogoro tunaungana  na Mwenyekti wa CCM  Dkt Magufuli kwanza tuitaka   dunia ijikinge na virusi  vya Corona. Pia  wito wetu dunia ikatae   fedheha inayoipa mateso zimbwebwe dhidi ya vikwazo vya kiuchumi kwa nchi hiyo na kutatiza "Alisema Shaka  

Aidha Katibu huyo alisema vikwazo hivyo vikiendelea kubaki ni kama kuifunga upya Zimbabwe minyororo inayominya uhuru  wake, kuinyima  fursa  muhimu huku   vikwazo hivyo vikiwa ni adhabu  na ukandamizaji  wa haki unaoinyemelea nchi hiyo ya  kusini mwa Afrika.

"Kuendelea kuwepo kwa vikwazo vya kiuchumi   ni kuilundikia mzigo wa  mateso Zimbabwe bila hatia .Kibinadamu haipaswi tena kuwashuhudia wazimbabwe wakiishi kwa mashaka huku nchi za sadc  zikiitazama nchi hiyo na watu wake wakiteketea kiuchumi na maradhi" Alisema 

Shaka  alisema  Rais Emerson Mnangagwa wa Zimbabwe haikustahili arithishwe vikwazo  hivyo badala yake ingekuwa uungwana akapewa  nafasi na fursa  ili atekeleze sera zake , kutoa  ushirikianao  kidiplomasia na kufanyakazi za kimahusiano na taasisi za kidunia.

"Ni vikwazo haramu vya kiuchumi vyenye  maonevu na fedhuli. Wakati huu dunia ilipaswa kujali  utu  wa kila mmoja duniani .Ni wakati wa kupambana na virusi vya Corona na kuonyesha mshikamano.  Vikwazo kwa zimbabwe  havijengi ustawi wala havina  maana yoyote " Alisisitiza Shaka 

Hata  hivyo  Katibu  huyo alisema ni jambo la kufurahisha kumuona Mwenyekiti  wa CCM  Rais Dkt Magufuli, akiendeleza   msimamo  wa  kupigania haki na utu  duniani huku ukizitaka  nchi  za sadc kusimama pamoja na kuzidisha ari ya mapambano na kupinga aina yoyote  ya ukandamizaji  haki
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com