METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, November 17, 2019

TPRI KUWAFUTIA LESENI WAFANYABIASHARA WATAKAOKIMBIA UKAGUZI WA BIASHARA ZA VIUATILIFU





Kaimu Msajili wa viuatilifu Tanzania Dr Joseph Bukalassa amepiga marufuku kitendo cha  uuzaji na usambazaji wa viuatilifu bandia,vilivyoisha muda wake na ambavyo havijakaguliwa na kusajiliwa kitendo ambacho amesema kinasababisha kuwepo kwa madhara kwa watumiaji,mimea na mazingira kwa ujumla.
    
Bukalassa ameyasema hayowakati wa kufunga mafunzo ya 51 ya matumizi sahihiu na salama ya viuatilifu yaliyotolewa kwa wadau waviuatilifu(wauzaji,wakulima,maafisa ugani wa serikali na wa sekta binafsi pamoja na wasambazaji wa viuatilifu)yenye lengo la kuwawezesha wafanyabiashara wa viuatilifu kutekeleza majukumu yao ya kibiashara kikamilifu ili waweze kuhudumia wateja wao kikamilifuna kuhakikisha kwamba maswala muhimu yanazingatiwa.Kuwahudumia wateja wao na kuwataarifu ni kiambato ganicha kiuatilifu kipo kwenye kiuatilifu hicho na kinafanya kazi gani pamoja na namna bora na salama ya kutumia kiuatilifu hicho ili waweze kuwasadaidia wale wanaoenda kupuliza moja kwa moja shambani
    
Aidha amesema kuwa kuuza na kusambaza viuatilifu visivyo sajiliwa ,bandia vilivyoisha muda wa matumizi au kufanya biashara ya uuzaji na usambazaji wa viuatilifu pasipo kukaguliwa na kusajiliwa ni sawasawa na kujiingiza kwenye mtego usio teguka

 “Vibali vyote hapa nchini husauiniwa na mimi sasa kunatabia ukiona wakaguzi wanahitaji kuklagua duka lako unawakimbia sasa mimi nisaini kibali chako alafu watu wangu unawakimbia inamaanisha kuwa hufai kufanya biashara hapa nchini usiingie kwenye huo mtego nakuhakikishia hautauza tena”amesema Dr Bukalassa

Kwa upande wake muwakilishi wa kaimu mkurugenzi mkuu TPRI,Dr Ester Kimaro ambae pia ndo alikuwa mgeni rasmi katika katika ufungaji wa mafunzo hayo amesemakuwa wafanyaji biashara za viuatilifukuzingati sheria za nchi kama zilivyo biashara nyingine.

Aidha ameongeza kuwa matumizi ya viuatilifu au biashara za viuatilifu zinaweza kusababisha madhara mbalimbali ya kiafya kwa watumiaji,jamii,wanyama na hata mazingira kwa ujumla kama zikifanywa bila kufuata taratibu na kanuni za matumizi sahihi ya viuatilifu hivyo,amewataka wahitimu wa mafunzo hayo kupeleka elimu waliyoipata kwa wiki mbili ya matumizi sahihi na salama ya matumizi ya viuatilifu na udhibiti endelevu wa visumbufu kwa jamiii ili kuepuka kuwepo kwa madhara hayo.

Pia amesemakuwa ni matarajio wa taasisis hiyo kuwa kutokana na elimu waliyo ipata watakwenda kuhamasisha matumizi sahihi na salama ya matumizi ya viuatilifu na udhibiti endelevu wa visumbufu ikiwemo kutokomeza uuzaji na usambazaji wa viuatilifu visivyo kaguliwa na sajiliwa na TPRI.

Amesemakuwa washiriki wa mafunzo hayo watakuwa na uwezo wa moja kutambua viuatilifu bandia,vilivyoisha muda wake na visivyo sajiliwa,mbili kutambua,kuainisha na kudhbiti magonjwa na wadudu wa mimea ya kilimo pamoja na wadudu waenezao magonjwa kwa binadamu na mifugo,tatu kujua aina mbvalimbali za mabomba na stadi za kutumimia mabomba ya unyunyuziaji viuatilifu,nne kujua aina mbalimbali za viuatilifu, kutambua athari za viuatilifu kwa binadamu,mifugo,mimea na mazingira.

Pia tano kusoma,kutasfiri mambo yote yaliyoandikwa kwenye vibandiko hivyo kuwasaidia kutoa maelekezo kwa watumiaji wa viuatilifu hususani wakulima,sita kujua namna ya kusajili biashara ya viuatilifu kwa njia rafiki na rahisi popote kwa kutumia teknolojia ya mtandao yaani ATMIS, sita kufanya biashara za usambazaji na uuzaji wa viuatilifu kikamilifu bila kuvunja sheria na ufukizaji wa mazao.

Kwa mujibu wa Bw Jumanne Rajabu mchambuzi mfawidhi wa viuatilifu ambae pia ndiye mratibu wa mafunzo hayo amesemakuwa mafunzo hayo yataleta tija katika Kilimo kwani wahitumu walio hitimu watakwenda kutoa huduma sahihi na salama kwa wakulima.

Aidha ameongezakuwa mafunzo hayo yanaendeshwa TPRI makao makuu Arusha kila wiki ya pili ya mwezi wa tano na kila wiki ya pili ya mwezi wa kumi na moja kila mwaka kwa wiki mbili na mikoani ambapo hufanyika kwa wiki moja hivyo ametoa wito kwa wauzaji,wakulima,maafisa ugani wa serikali na wa sekta binafsi pamoja na wasambazaji wa viuatilifu kuhudhuria wanaposikia kunamafunzo mikoani na hayo yanayo fanyikia makao makuuu Arusha.

Amemalizia kwa kusemakuwa sheria inawataka wauzaji na wasambazaji wa viuatilifu kupata mafunzo kabla ya kuanza kufanya biashara hivyo amewaasa wanaotaka kufunzgua biashara hivyo ili waepukane na usumbufu kutoka kwa mamlaka yaani wakaguzi wa biashara za viuatilifu wa mara kwa mara wafike kupata mafunzo na vyete ambavyo vitawasaidia kwenye kufanya usajili wa biashara zao.

MWISHO
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com