Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwa
na Mkewe, Marry Majaliwa (wapili kulia) akisalimiana na Naibu Waziri wa
Viwanda na Biashara, Stela Manyanya, wakati akiwasili kwenye uwanja wa
Bombadia Singinda, kufungua maadhimisho ya Wiki ya Viwanda Kitaifa,
Oktoba 6.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,
akikata utepe , kufungua maadhimisho ya Wiki ya Viwanda Kitaifa, kwenye
uwanja wa Bombadia mjini Singinda, Oktoba 6.2019. (Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu).
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwa
na Mkewe, Marry Majaliwa (kulia) akifafanuliwa jambo na Afisa Masoko
Mwandamizi wa TBS, Gladness Kaseka, wakati alipotembelea mabanda, katika
ufunguzi wa maadhimisho ya Wiki ya Viwanda Kitaifa, yaliyofanyika
kwenye uwanja wa Bombadia mjini Singinda, Oktoba 6.2019. Kushoto ni
Afisa Mkaguzi TBS, Domisiano Rutahala. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,
akiangalia mbegu ya kisasa ya alizeti, kwenye banda la Chama cha
Wasindikaji Mafuta wa Mkoa wa Singida (SISUPA), wakati alipotembelea
mabanda, katika ufunguzi wa maadhimisho ya Wiki ya Viwanda Kitaifa,
yaliyofanyika kwenye uwanja wa Bombadia mjini Singinda, Oktoba 6.2019.
Anayetoa ufafanuzi (katikati) ni Mwenyekiti wa Wasindikaji hao, Juma
Mene. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,
akifafanuliwa jambo na Meneja wa Kituo cha Kuendeleza Teknolojia (SIDO),
Arthur Ndedya, wakati akitembelea banda la SIDO, katika ufunguzi wa
maadhimisho ya Wiki ya Viwanda Kitaifa, yaliyofanyika kwenye uwanja wa
Bombadia mjini Singinda, Oktoba 6.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
0 comments:
Post a Comment