![](https://fullshangweblog.co.tz/wp-content/uploads/2019/10/index-51-1024x683.jpg)
Afisa Kilimo wa wilaya ya Mpwapwa,
Edson Kileo,akizungumza wakati Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Tawala za
Mitaa chini(ALAT), Elirehema Kaaya alipofanya ziara ya kukagua
maendeleo ya mradi unaoendelea wa uboreshaji kituo cha
Kilimo,Mawasiliano na Taaluma cha mafunzo ya kilimo Kibakwe wilayani
humo.
![](https://fullshangweblog.co.tz/wp-content/uploads/2019/10/1-82-1024x683.jpg)
Mkuu wa kituo hicho Samson German
akisoma taarifa kwa upande wa kulia ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Tawala
za Mitaa chini(ALAT), Elirehema Kaaya akimsikiliza wakati alipofanya
ziara ya kukagua maendeleo ya mradi unaoendelea wa uboreshaji kituo cha
Kilimo,Mawasiliano na Taaluma cha mafunzo ya kilimo Kibakwe wilayani
humo.
![](https://fullshangweblog.co.tz/wp-content/uploads/2019/10/2-66-1024x683.jpg)
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Tawala
za Mitaa chini (ALAT), Elirehema Kaaya ,akikagua miradi huku Mkuu wa
kituo hicho Samson German akimuonyesha jinsi gani mbogamboga zinazolimwa
wakati alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya mradi unaoendelea wa
uboreshaji kituo cha Kilimo,Mawasiliano na Taaluma cha mafunzo ya kilimo
Kibakwe wilayani humo.
![](https://fullshangweblog.co.tz/wp-content/uploads/2019/10/2A-1024x683.jpg)
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Tawala
za Mitaa chini(ALAT), Elirehema Kaaya ,akiendelea na ukaguzi wa
maendeleo ya mradi unaoendelea wa uboreshaji kituo cha
Kilimo,Mawasiliano na Taaluma cha mafunzo ya kilimo Kibakwe wilayani
humo.
![](https://fullshangweblog.co.tz/wp-content/uploads/2019/10/3-50-1024x683.jpg)
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Tawala
za Mitaa chini (ALAT), Elirehema Kaaya, akitoa maelezo kwa Mkuu wa
kituo hicho Samson German wakati alipofanya ziara ya kukagua maendeleo
ya mradi unaoendelea wa uboreshaji kituo cha Kilimo,Mawasiliano na
Taaluma cha mafunzo ya kilimo Kibakwe wilayani humo.
…………………….
Na.Alex Sonna,Mpwapwa
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Tawala
za Mitaa nchini (ALAT), Elirehema Kaaya,amewataka vijana kukitumia
kituo cha kilimo,Mawasiliano na Taaluma kilichopo Mpwapwa mkoani Dodoma
kupata ujuzi wa kilimo cha mbogamboga na maua ili waweze kuondokana na
tatizo la ajira.
Hayo ameyasema jana wakati
alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya mradi unaoendelea wa uboreshaji
kituo hicho cha mafunzo ya kilimo Kibakwe wilayani humo.
Bw.Kaaya alisema kuwa mradi huo
umetumia zaidi ya Sh.Milioni 240 huku Halmashuari ya Mpwapwa ikitoa
zaidi ya Sh.Milioni 90 na kwamba ni miongoni mwa miradi wa kuboresha
mazingira ya biashara na uwekezaji(LIC) unaotekelezwa kwenye mikoa ya
Dodoma na Kigoma kwa ushirikiano kati ya Ofisi ya TAMISEMI na ubalozi wa
Denmark.
Aidha amewashauri vijana wanaomaliza kidato cha nne kujifunze kwenye kituo hicho ili kuondokana na malalamiko ya kukosa ajira.
Bw.Kaaya alisema kuwa hakuna
ajira,lakini wajue hakuna ajira inayozidi kilimo cha aina hii, hii elimu
wanayopata hapa wakaifanye wakati wanasubiri matokeo ya kuendelea na
elimu ya juu.
Alisema kuwa kumekuwa na mwamko
mdogo wa vijana kuchangamkia mafunzo yanayotolewa na kituo hicho na
wengine kuona kama kilimo ni utumwa wakati kinaweza kuwakwamua kiuchumi.
Hata hivyo Kaaya ,aliagiza
kujengwa kwa mfumo wa kuvuna maji ya mvua kwenye majengo ya kituo hicho
ili kukabiliana na upungufu wa maji kwenye eneo hilo.
Alisema kuwa changamoto iliyopo
katika kituo hiki ni kutokuwa na maji ya kutosha,uzio na kutokuwa na
nguvu kazi wakihitajika vibarua hawapatikani,”alisema.
Awali, Mkuu wa kituo hicho Samson
German akitoa taarifa alisema kituo hicho kinatoa huduma za kilimo na
mifugo kwa wakulima katika eneo husika.
Alisema changamoto iliyopo
ni vijana wanaozunguka eneo la kituo hicho kutotaka kujishughulisha
kufanya kazi hasa shughuli za kilimo.
“Mpaka sasa kituo kimetoa elimu
kwa vitendo kwa wanafunzi 30 wa mafunzo ya ujuzi waliotoka chuo cha
kilimo na mifugo Visele Mpwapwa, pia wakulima 60 kutoka vijiji vya
Kibakwe, Iyenge na Chamtumile juu ya kanuni za kilimo bora cha
mbogamboga ili kuboresha lishe na kuongeza kipato,”alisema German
Naye, Afisa Kilimo wa wilaya ya Mpwapwa, Edson Kileo alisema kuna mwitikio mdogo kwa wakulima kujifunza.
0 comments:
Post a Comment