METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, October 1, 2019

DKT TULIA ACHANGIA SEKTA YA ELIMU MKOANI MBEYA

 Naibu Spika Dr. Tulia Ackson kwa kupitia taasisi yake ya Tulia Trust amefanya ziara katika shule mbalimbali mkoani Mbeya lengo likiwa ni kusaidia kuboresha miundombinu ya elimu ambapo miongoni mwa shule hizo ni pamoja na Shule ya msingi Jitegemee ambayo ameipa mchango wa Shilingi Milioni mbili (Tsh 2,000,000/-) ili kusaidia ukarabati wa miundombinu mibovu katika shule hiyo.
Pia, baada ya kusomewa changamoto nyingine zikiwemo ubovu wa madarasa, ukosefu wa uzio na ofisi za waalimu, Dr. Tulia ameahidi kutoa msaada zaidi kwenye shule hiyo kwa kupitia taasisi yake ya Tulia Trust.
Katika hatua nyingine, Dr. Tulia ametoa mchango wa Shilingi Milion moja na laki sita (Tsh 1,600,000/-) katika Shule ya Msingi Nzovwe iliyopo Jijini Mbeya ili kusaidia pia uboreshaji wa miundombinu isiyo rafiki katika shule hiyo ambapo pia alisomewa changamto zingine ikiwemo ubovu wa madarasa, uzio wa shule n.k
“Nimesomewa changamoto nyingi zilizopo katika shule zetu hizi ambapo niseme tu sisi kama Tulia Trust tumezipokea na tutaenda kuona ni namna gani basi tunaweza kuzifanyia kazi ili basi watoto wetu hawa waweze kuzoma katika mazingira yaliyo bora na salama”-Dr. Tulia
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com