METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, September 15, 2019

VIJANA WA CHAMA CHA MAPINDUZI TAWI LA CBE SOKOINE WAJITOKEZA KUFANYA USAFI NA KUTOA MSAADA JIJINI MWANZA



Vijana wa Chama Cha Mapinduzi tawi la SOKOINE CBE leo wamejitokeza na kufanyaa usafi katika kitu cha Afya Buzuruga, ilikiwa Lengo  ni kuwawezesha vijana kujijengea uwezo wa kuweza kushiriki shughuli za kijamii na kutengeneza mwamko wa kuona kua wao wana jukumu la kuhakikisha kuwa wanakuwa kiigizo chema katika jamii.

Usafi huoo uliambatana na zoezi la utoaji msaada kwenye wodi ya akina mama na watoto pia na kwa wagonjwa wengine walio lazwa  hospitali hapo.

Sambamba na hilo pia wasomi hao waliweza kupima afya zao(HIV). hili lilikuwa ni kuonesha umuhimu wa kuweza kujua hali za afya zao na kuwa kielelezo kwa jamii kwa kuwaonyesha wananchi umuhimu wa kujua afya zao.
Akizungumza na wanachuo  hawa wa CBE mganga mfawidhi wa Dkt. Mange aliwashukuru kwa kuweza kuja kufanya usafi katika kituo hicho kwan mara kadhaa wamekuwa wakielemewa katika kuhakikisha usafi unafanyika kwa muda kutokana na uhaba wa vifaa na wafanyakazi.

Pia ameishukuru serikali kwa ajili ya fedha mln 400 za mradi wa majengo ili kuwezesha urahisishaji wa huduma kwa wananchi. Lakini kuweza kujiandaa na uchaguzi wa serikali za mitaa utakao fanyika mwaka huu.

Suala la kujitolea kufanya usafi katika maeneo ya hospitali limekuwa likufanywa na vikundi vichache katika jamii,ukilinganisha na kwamba bado maeneo hayo yanahitaji uwepo wa wananchi wanaojitolea,licha ya hilo wagonjwa waliopo hospitali wanahitaji faraja kutoka kwa wanajamii panapopatikana kikundi au vikundi vya kwenda kuwaona ni vyema.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com