METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, September 28, 2019

PICHA ZA MATUKIO ZIARA YA WAZIRI KAIRUKI MGODI WA MADINI YA GRAPHITE RUANGWA -LINDI

Naibu Waziri ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angeline Mabula akizungumza jambo wakati wa kikao cha majumuisho cha ziara ya kutembelea miradi ya uwekezaji katika Wilaya ya Ruangwa mkoni Lindi pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika masuala ya Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki (aliyekaa kulia) kilichofanyika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo.
Meneja wa Kampuni ya Uchimbaji madini ya Lindi Jumbo Paul Shauri akionesha michoro ya muonekano wa eneo la mgodi wa madini aina ya uno (Graphite) wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika masuala ya Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki pamoja na Naibu Waziri ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angeline Mabula.
Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Bw. Hashim Mgandilwa akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa kikao hicho cha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika masuala ya Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki pamoja na Naibu Waziri ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angeline Mabula katika ofisi zake Mkoani Lindi.
Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Ruangwa Bw. Barnabans Essau akisalimia wakati wa kikao hicho.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika masuala ya Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki pamoja na Naibu Waziri ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angelline Mabula wakiwa katika ziara ya kukagua eneo lililotengwa kwa ajili ya uchimbaji wa madini aina ya uno (Graphite) lililopo Wilayani Ruangwa Lindi Septemba 27, 2019.
(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com