METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, February 9, 2019

PESA ZA MBUNGE ROSE TWEVE ZAGEUKA LULU KWA AKINA MAMA WA KATA YA NZIHI MKOANI IRINGA


Baadhi ya wajumbe wa kikundi cha Rose Tweve kilichopo kata ya Nzihi mkoaniri Iringa wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kikao chao cha kikatiba  

 NA FREDY MGUNDA

Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Rose Tweve ameendelea kuitunisha mifuko ya wanawake wa UWT mkoa wa Iringa kwa kukuza mtaji walipewa  awali na mbunge huyo.
 
Akizungumza na blog hii mwenyekiti wa kikundi cha Rose Tweve, Aulelia Mbembe alisema mbunge wa viti maalum Rose Tweve aliwapa mtaji wa shilingi laki tano(500,000/=) kwa kuanzia lakini waliunda kikundi na kukiita Rose Tweve kwa lengo la kumuuezi mbunge huyo kwa mchango wake kwa wanawake wa UWT kata ya Nzihi mkoani Iringa.

“Mbunge alitupa mtaji lakini tulijiongeza  kwa kukopeshana kwa riba ndogo ambayo tulijipangia sisi wenyewe  kwa kukopeshana na kukutana kwa mwezi mara moja kwa ajili ya kununua hisa pamoja na kubadilisha mawazo kwa lengo la kukuza mitaji na kufanya maendeleo yetu binafsi” alisema Mbembe 

Mbembe alisema kuwa mtaji wa kikundi cha Rose Tweve kimefanikiwa kukuza mtaji kutoka shilingi laki tano 500,000/=) hadi kufikia kiasi cha shilingi milioni kumi laki moja na nusu (10,150,000/=) kwa kipindi cha miaka mitatu kutoka mwaka 2017 hadi hii leo hapo ndio utajua kuwa ukimwezesha mwanamke unakuwa umeikomboa jamii.

‘’Kama kikundi tunategemea  kuja kuwa  na miradi yetu mikubwa itakayokuwa inaingiza faida kwetu na taifa kwa ujumla kupitia kulipa kodi kwa miradi hiyo ,lakini tunategemea  kutembelea  na kusaidia vikundi vya watu maalumu kama vile walemavu ,yatima ,wazee wasiojiweza,na waathirika wa vvu,yote haya  ni mchango na matunda ya Mbunge Rose Tweve ,kwa kweli shukrani  nyingi zifike kwake ,na viongozi wengine wachukue mfano  wa mbunge dada Rose Tweve kwa kusaidia  jamii kama Rose Tweve alivyotusaidia sisi  kikundi cha akiba cha wanawake(UWT) Rose Tweve Nzihi ‘’Alisema Aulilelia Mbembe mwenyekiti wa kikundi hicho.

“Hebu angalia ndugu mwandishi wa habari jinsi gani wanawake wa UWT kata ya Nzihi tulivyoweza kutumia vizuri fursa tuliyoipata kutoka kwa mbunge Rose Tweve kwa kutusaidia kubadilisha maisha yetu kwa kuweza kujikimu kimaisha tofauti na ilivyokuwa hapo awali hivyo tunamshukuru sana mbunge Rose Tweve” alisema Mbembe

Mery  Msigara  ni moja wa wajumbe wa kikundi cha akiba cha Rose Tweve  alisema kuwa alikuwa anashinda nyumbani  kwa kumtegemea mume wake kwa kila kitu lakini baada ya kujiunga kwenye kikukidi cha Rose Tweve amekuwa mjasiriamali  anayeweza kufanya biashara ndogondogo na kupata faida kila kukicha huku familia yake ikipata maendeleo ukilinganisha na awali,yote haya ni matunda ya mbunge Rose Tweve.

Wajumbe katika kikundi hicho wameonekana  kuwa na malengo makubwa katika kufanikiwa huku wakisema kwa mwanga waliooneshwa na  mbunge Rose Tweve wanaamini watafikia malengo yao ya mbali kimafanikio kupitia kikundi hicho cha akiba cha Rose Tweve .

Hadi sasa mbunge Rose Tweve amefakiwa kuvifikia na kuvitembea jumla ya vikundi 92 vya mkoani iringa na kuviwezesha kama ilivyo kwa hiki kikundi cha kata ya Nzihi. 
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com