METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, December 12, 2018

MHE BASHUNGWA AKUTANA NA TBL KUJADILI NAMNA YA KUFUNGAMANISHA KILIMO NA VIWANDA

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa (Mb) akiongoza kikao kazi kilichofanyika katika ofisi za wizara ya Kilimo maarufu Kilimo 1 Jijini Dar es salam leo tarehe 12 Disemba 2018 wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Ununuzi na Ugavi wa Afrika Mashariki wa kampuni (TBL) Ndg Gareth Da Gee.
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa (Mb) akiongoza kikao kazi kilichofanyika katika ofisi za wizara ya Kilimo maarufu Kilimo 1 Jijini Dar es salam leo tarehe 12 Disemba 2018 wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Ununuzi na Ugavi wa Afrika Mashariki wa kampuni (TBL) Ndg Gareth Da Gee.

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Ununuzi na Ugavi wa Afrika Mashariki wa kampuni (TBL) Ndg Gareth Da Gee kujadili namna ya kufungamanisha Kilimo na Viwanda.

Amesema kuwa kampuni hiyo inazalisha bia kwa wingi nchini Tanzania hivyo mazungumzo hayo yataongeza chachu na tija katika kuongeza masoko ya wakulima nchini.

Mhe Bashungwa ameyasema hayo leo tarehe 12 Disemba 2018 wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika ofisi za wizara ya Kilimo maarufu Kilimo 1 Jijini Dar es salam na kuhudhuriwa pia na Kaimu Mkurugenzi wa sera na Mipango, Kaimu Mkurugenzi wa idara ya usalama wa chakula, Kaimu Mkurugenzi wa idara ya maendeleo ya mazao.

Wengine ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya utafiti Tanzania (TARI), Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya Kilimo (TADB) na Benki ya Uwekezaji (TIB), Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko, na Muwakilishi wa Baraza la uwezeshaji wananchi kiuchumi.

Katika kikao hicho Mhe Bashungwa amesema kuwa mazungumzo hayo yataongeza mtazamo wa jumla kwa wakulima nchini kujipatia masoko ya mazao ya mvinyo hususani mahindi, Shairi, Ngano, Sukari na Mtama.

“Alisema kuwa kwa zao la mahindi pekee nchini wakulima wana ziada ya Tani 810,000 huku bei ikiwa chini hivyo Bodi ya Nafaka na Mazao mchanganyiko wanapaswa kukutana na TBL ili kuangalia mahitaji yao kwenye mahindi na kuzingatia ubora ili wakulima waweze kunufaika na fursa hiyo” Alikaririwa Mhe Bashungwa

Alisema kuwa moja ya mikakati ya serikali ya awamu tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli ni pamoja na kutafuta masoko ya mazao ya wakulima nchini ili wakulima hususani wa mazao ya shairi, mahindi, ngano, sukari na mtama waweze kunufaika na kilimo.

Vilevile ameipongeza kampuni ya Bia ya TBL kwa kuanza kufanya utafiti kwenye zao la muhogo na zabibu kwani wakulima wa mazo hayo wataongeza uzalishaji wa mazao hayo nchini.

Bashungwa amesema kuwa serikali inaendelea na mkakati wake wa kuimarisha masoko ya wakulima nchini ambapo atakutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa viwanda vingine.

MWISHO.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com