METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, December 15, 2018

BILIONI 133.2 ZIMEKWISHALIPWA KWA WAKULIMA WA KOROSHO – MHE HASUNGA


Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Mtwara

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amesema kuwa mpaka kufikia jana tarehe 14 Disemba 2018 wakulima 130,163 wamelipwa jumla ya shilingi 133,259,933.855

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga ametoa takwimu hizo tarehe 15 Disemba 2018 wakati akizungumza kwenye mkutano wa wabanguaji uliofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.

Alisema kuwa katika Mkoa wa Mtwara wananchi ambao wamekwishalipwa ni 77,055 huku jumla ya fedha iliyolipwa ni Bilioni 80,098,982,060  

Katika mkoa wa Lindi tayari wakulima 41,564 wamekwishalipwa kiasi cha Bilioni 42,502,635,227 huku katika mkoa wa Ruvuma wakulima 11,463 wamekwishalipwa kiasi cha Bilioni 10,557,222,943

Aidha, Mhe Hasunga amesema kuwa katika mkoa wa Pwani Milioni 101,091,960 zimekwishalipwa kwa wakulima 81

Alisisitiza kuwa vyama vilivyohakikiwa ni 461 na vilivyolipwa ni 451, ambapo jumla ya Kilo 40,381,798 zilizolipiwa.

MWISHO
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com